Sunday, August 30, 2015

Ssentongo awaita mezani Simba


UNAKUMBUKA Robert Ssentongo? Huyu jamaa kwasasa ndiye mtambo wa mabao katika kikosi cha URA ya Uganda.

Miaka kumi iliyopita alikuwa akisakata soka pale Msimbazi, katika kiwango cha juu kabisa, lakini pilikapilika za pale zikamtoa nje akaondoka.

Miaka kumi baadaye mchezaji huyo yuko katika kiwango kile kile, akiwa na makali yaleyale.
Ssentongo amesikia Simba wanasaka straika wa maana wa kuwatoa kamasi mabeki na kufunga mabao, akacheka kidogo, kisha akauliza; “Mimi hawanioni?”.

Ssentongo amesema kwamba anakaribisha ofa kutoka Simba kwasababu ni timu anayoipenda, na kwamba kama watakubaliana anaweza kusaini Simba na akaifanyia makubwa.

“Najua muda wenyewe umemalizika, lakini kama wangekuja mapema tukaongea ningejiunga na Simba, nikaanza maisha mapya. Mimi najitambua kwamba ni aina ya washambuliaji ambao Simba inawataka kwasasa”, amesema.

Mshambuliaji huyo ambaye mwaka 2009 alirejea tena Tanzania na kujiunga na African Lyon amesema kwamba pamoja na kwamba amesakata soka kwa muda mrefu, lakini kiwango chake kiko juu.

No comments:

Post a Comment