Sunday, August 30, 2015

Simba yafunga usajili na wawili

DIRISHA la Usajili kwa timu za Ligi Kuu Tanzania bara linatarajia kufungwa Jumapili (Leo) saa 6:00 usiku huku uongozi wa klabu ya Simba ikitangaza kukamilisha kumalizana na wachezaji wawil raia wa kigeni.

Taarifa za uhakika ambazo Mwanasoka linazo zimebainisha kuwako kwa hatua za mwisho za uongozi wa Rais wa klabu hiyo, Avans Aveva kukamilisha mazungumzo ya kuwasainisha wachezaji hao wawili wa maana.

Akinukuliwa jana, bila ya kutaja majina ya wachezaji hao, Aveva alizungumza kwa uhakika mkubwa kuwa, wachezaj hao ni wale watakaokubalika pia na benchi la ufundi ambalo ndilo lililo na jukumu la kuamua nani asajiliwe na yupi wa kuachwa.

Rais huyo, alisema, uongozi una masaa machache ya kupokea baraka za benchi la ufundi juu ya wachezaji hao kabla ya kuweka bayana majina ya wachezaji hao na kuungana na wenzao ambao tayari wameshasaini kandarasi ya kukukipiga Msimbazi msimu mpya wa ligi.

Ingawa ni mapema mno, lakini mwandishi wa habar hizi amebainishiwa majina yao na kuumbwa kubakia kuwa ni suala la siri hadi hapo kila kitu kitakapokwenda sawia bin sawa.

Pamoja na usiri huo, Mwanasoka linatambua kuwapo kwa majina ya wachezaji wawili raia wa kigeni ambao tayari wapo katika malengo ya kusajiliwa baada ya kufuzu majaribio chini ya kocha Dylan Kerr.

Wachezaji waliomo ndani ya kurunzi za majaribio katika kambi ya Wekundu hao kisiwani Unguja ni pamoja na Pape Abdoulaye N'Daw ambaye tayari ameanza kuangalia kiwango, huku mwenzake Makan Dembele alitarajiwa kutua viswani humo muda wowote.

"Tutakamilisha usajili wetu katika ubora mkubwa ila kwa kupata baraka za kocha wetu Dylan Kerr ambaye ndiye anayesubiriwa, lakini kila kitu kinakwenda sawa kabla ya kufungwa kwa dirisha la usajili wa wachezaji wa kigeni".

"Tunaamini kila mwanasimba atafurahia kikosi cha msimu huu na hilo ndilo linaufanya uongozi kuwa kufanya mambo yake katika umakin mkubwa kwa kusikiliza maoni ya makocha wetu Kerr (Dylan) na Matola (Seleman)".

Alinukuliwa mjumbe mmoja wa kamati ya usajili ambaye hata hivyo hakutaka jina lake liandikwe kwasababu ya kuheshimu mipaka ya majukumu.

Akizungumzia masuala ya ufundi, mjumbe huyo alisema, wachezaji wote wawili wana uwezo wa kufunga mabao ya masafa marefu, sifa ambayo imewavutia makocha wote wawili

No comments:

Post a Comment