Saturday, August 29, 2015

Henry atoa maneno mazito

Thierry Henry Barcelona

Thiery Henry: “I went to sleep knowing what to do. I always thought if I don’t move, Abidal won’t, Iniesta won’t get the ball. It’s constant.”
Hayo Ni maneno ya Thierry Henry Na Mimi Yamenikosha sana  na nimeona ngoja nitie maneno yangu  kuzungumzia kuhusu mpira wa miguu…
Unajua kwa sisi mashabiki wa mpira tunaishia tu kujua kuhusu formation za team labda sana ukijitahidi utajua kuhusu filosofi flani ya timu flani basi hapa tumekua tumeridhika na tuna-enjoy mpira kwa kiasi kile  tunachouelewa …
Ila mpira kama mpira una utaalamu wake ambao watu wengi  hua hatuufahamu wala hatujishughulishi kuujua ambao labda utaalamu huu ungeweza kutubadili mawazo na kutuongezea sana radha ya soka.
Kitu kinacholeta ladha ya mpira na utofauti wa timu moja na nyingine sio tu pekee filosofi ya timu na wala sio tu formation pekee inayotumiwa na timu .. utofauti wa team moja hadi nyingine unaletwa na jinsi gani utautembeza mpira wenu kutoka sehemu moja kwenda nyingine kutumia watu gani na ni kwanini mtu au watu hao  ndio watumike, kumbe basi timu zinaweza kushare formation moja, na pia zinaweza kushare filosofi moja ya mpira ila bado njia zao za kupitisha hiyo mipira kutoka eneo moja hadi lingine zikawa tofauti.
Na kutokana na hili suala ndio maana kuna muda hata zile team kubwa zenye wachezaji wazuri hua zinafungwa. Kinachowafanya wafungwe hapa sio formation na wala sio kwakua mchezaji flani anacheza mahali flani ndio maana timu imefungwa kwakua sio nafasi yake, bali kinachofanya kupoteza mechi ni mbinu za kupitisha mipira za timu husika ilioshinda.
Ukisikia neno ‘Game Plan’ hua haliishii tu kwenye formation na filosofi za timu basi, kama ingekua inaishia hapa basi makocha wenye experience zao au wale high profile managers wasingekua wanajisumbua kwenda uwanjani kuisoma timu pinzani ikicheza na timu nyingine kwakua kutokana na experince zao wangeelewa tu wacheze nazo vipi hizo timu wakikutana nazo kwakua mara nyingi hua wanajua vitu vingi sana kweye soka.
Na pia mnaweza mkakutana na timu mbili tofauti mnacheza mpira unaofanana na formation inayofanana ila bado matokeo yakawa tofauti hii ni kutokana na hamuwezi kufanana njia za kupitisha mipira wachezaji mnaotumia kuanzisha mashambulizi wapo kwenye position zipi na pia ni mchezaji gani anaanza kukaba wapi, hadi kufika wapi mnaanza kungia kwa nguvu kuchukua mpira, mnaiba vipi muda kuvizia kuanzisha shambulizi hamuwezi kufanana hivi vitu.
Makocha wanakua wana njia nyingi za kuwaambia wachezaji wao wapitishe mipira kutokana mechi husika pamoja na uwezo wa wachezaji waliokuwepo uwanjani siku hiyo, hivyo basi kila mechi hasa hizi mechi muhimu hua zina game plan yake ya tofauti ambayo hii ni zaidi ya kuona formation uwanjani. Makocha wanaamua kwenda viwanjani kuangalia mpinzani anavyocheza  kwakua huwez kuiona game plan ya mpinzani wako kwenye TV kwakua TV zinaonesha tu sehemu ambao mpira ulipo.
Mpira hua unachezwa sehemu mbili yule anaekua na mpira kwa wakati huo pamoja na wale wasiokua na mpira ina maana positioning zao ni jinsi gani timu inajipanga kama mpira wanao wao,  ni mchezaji gani hua anakimbia kwenye eneo gani kama team yake ina mpira hivi ndio vitu ambavyo makocha au scouts wanaenda kuvitazama uwanjani ambavyo huwezi kuviona kwenye TV, TV itakuonesha mpira ulipo mara mchezaji kapokea pasi alipotokea huwezi kuona labda hadi replay .
Henry anakwambia alikua anaenda kulala akijua kua ili Abidal aweze kuachia mpira miguuni mwake lazima yeye awe amefika eneo fulani na asipofika hilo eneo ina maana Abidal hawez kuachia mpira hapa ikumbukwe kua mpira huu ambao upo kwa Abidal hautoki miguuni kwa Abidal moja kwa moja hadi kwa Thierry Henry la hasha ila unapitia kwa Iniesta ambae nae kwa wakati huo anakua hana mpira kwakua mpira upo miguuni kwa Abidal.
Mpaka hapa kuna kua kuna watu watatu wanacheza mpira mmoja ambao upo miguuni mwa mtu mmoja tu ambae ni Abidal.
Kama Thiery Henry asipofanya hii move anaweza kuisababishia timu yake iwe in trouble kwakua anaweza kufanya Abidal asifanye maamuzi sahihi kama ilivyokua planned, kwaiyo Henry akifanya move yake na Iniesta yeye kazi yake inakua kumtupia tu Henry kwakua anajua ni wapi alipo, hapa sasa Iniesta anaweza akakupumbaza labda kwa kupiga chenga mbili tatu ili akushawishi kua ana mpa Henry labda tu kwakutaka kuuachia mpira miguuni mwake kwakua amekabwa kumbe anakua anakudanganya Thierry Henry ndio anakua mtu sahihi alitaka kumpa.
Hapa ndio mpira hua unachezwa na ndio maana kwa watu wenye uelewa haachi kwenda kuangalia mpira uwanjani hata kama unaoneshwa kwenye TV kwakua akienda uwanjani anaona mchezo mzima ulivyo.
Hizi formation zipo ili tu wachezaji wakae kwenye system flan ila kinachofanya team ifungwe au ipate ushindi sio tu formation pekee mpira hua hauishii hapo ni ile game plan ndio inayosababisha timu kufungwa au kushinda.
Kuna muda unaweza kuona timu ile ile moja na wachezaji wanajipanga vile vile kwenye mechi kama tano mfululizo na mechi zote timu hiyo hiyo moja kwa kikosi kile kile inapata matokeo ya ushindi, kumbe basi hapa wanachokua wanabadilisha ni jinsi gani ya kucheza, kupitisha ile mipira yao wakati wa kushambulia na style yao ya kuzuia wakati wa kukaba.
Kwa maana hii basi ni kwamba hamna timu yeyote duniani hata kama iwe bora kiasi gani inayoweza kucheza yenyewe tu bila mwalimu wa kuwaelekeza, na ndio maana hata wale wachezaji magwiji kabisa waliowahi kuwa bora duniani hua na wao wanaenda kusomea kua walimu wa mpira.
Sisi mashabiki wa mpira tunakua rahisi mno kusema na kulalamika “mchezaji flani hawez kucheza kama mchezaji wetu flani, mara me huyu flani anaudhi sana kocha nae kwanini hamtoi anaendelea tu kumpanga mi naudhika” *** tambua kama hata wewe umeona flani hawezi kucheza kama flani aliekua benchi basi ujue hata mwalimu anaewafundisha wachezaji hao amewaona na anawajua kuwa flani hajui kufanya kitu hiki na isitoshe anakua nao kila siku mazoezini.
Makocha wote duniani wanaangalia zaidi game plan zao kuliko uwezo wa mchezaji mmoja mmoja, ndio maana kwa wanaojua soka wanakwambia kujua mpira na kudumu kwenye mchezo wa mpira sio kipaji tu unaweza ukawa na kipaji na usifike popote, muhimu ni kufanya mazoezi kujituma sana na kuwa na nidhamu kweli kweli nje na ndani ya uwanja na pia kufata maelekezo ya mwalimu hapa utafanikiwa kimpira.
Ukimkuta mchezaji mwenye kipaji cha ukweli, na ana nidhamu ya hali ya juu anafanya mazoezi kisawasawa na kusikiliza walimu wao hawa ndio hua wanafanikiwa mno.
Kwaiyo ushauri wangu kwa watu wa mpira ni kwamba, tunapoenda kuangalia mpira kabla hujaanza kulalamika kwanini flani anachezeshwa hivi kwanini flani hachezi na kuanza kukasirika, jaribu kutafakari kwanza ni nini kocha ana hitaji kutoka sehemu hiyo, kama ukitafakari na ukaelewa labda inaweza kukusaidia kuenjoy huo mchezo badala ya kukasirika na itakusaidia pia kuelewa.
Na hata hao wanaokua nje haina maana watakaa nje forever, kuna wakati inakua wanakua wanamechi zao watacheza au labda pia walimu wao wanakua wanawatafutia njia ya kuwaingiza kikosi cha kwanza bila kuharibu muendelezo wa timu.
Naishia hapa namalizia kwakusema kua nimekoshwa sana na maneno ya Thiery Henry sentensi chache tu ila zimebeba maana nzima ya football.

No comments:

Post a Comment