Thursday, August 6, 2015

HAJIBU, KIIZA, WAIONGOZA SIMBA KUUA MECHI YA TANO MFULULIZO VISIWANI ZANZIBAR

simbaa
Klabu ya wekundu wa msimbazi imehitimisha mechi za kirafiki visiwani Zanzibar kwa kushinda mchezo wake wa leo iliyocheza dhidi ya KMKM kwa kuichapa klabu hiyo goli 3-2 mchezo uliopigwa kwenye uwanja wa Amaan Zanzibar ukiwa ni mchezo wake wa tano na kufanikiwa kushinda michezo yake yote ya kirafiki iliyocheza ikiwa visiwani humo.
KMKM ndio walikuwa wakwanza kufunga magoli yote mawili kupitia kwa mchezaji wao Mateo Antony Simon akifunga magoli hayo dakika ya 20 na 25 ya mchezo huo lakini Hamisi Kiiza ‘Diego’ akaipatia Simba goli la kwanza dakika ya 42 kipini cha kwanza na kuufanya mchezo huo kwenda mapumziko huku KMKM ikiwa mbele kwa goli 2-1.
Kipindi cha pili Simba walianza kwa kasi kubwa na KMKM wakaonekana wakiwa wamechoka na kushindwa kuendana na kasi ya Simba, ambapo mshambuliaji chipukizi wa Simba Ibrahih Ajib aliifungia klabu yake mabao mawili ya harakaharaka dakika ya 75 na 78 akaipa ushindi klabu hiyo wa goli 3-2. Mabao hayo yakiwa yamechangiwa na kiungo Mwinyi Kazimoto na kiungo aliyesajiliwa kutoka Zimbabwe Jastice Majiva.
Kesho Simba inatarajiwa kurejea jijini Dar es Salaam ambapo ilicheza mechi tano za kirafiki ikiwa visiwani Zanzibar. Mcheo wa kwanza Simba ilishinda kwa goli 2-1 dhidi ya Kombaini ya Zanzibar, mechi ya pili Simba ikashinda kwa goli  4-0 wakati mchezo wa tatu ilicheza dhidi ya Polisi ya Zanzibar na kushinda kwa goli 2-0 huku mchezo wake wa nne ikishinda pia kwa goli 3-0 mbele ya Jang’ombe na kumaliza na ushindi wa goli 3-2 dhidi ya KMKM.

No comments:

Post a Comment