Sunday, August 23, 2015

Matola amtaja Messi mpya Msimbazi


SELEMANI Matola
WASHABIKI wa  klabu ya soka bila  shaka walikuwa na maswali mengi pindi alipoondoka Ramadhani Singano 'Messi' na  kuna  baadhi walikuwa na shaka na pengo lake, lakini  njoo uangalie vita ya namba ya nafasi ya  winga, ndipo  utakapokubali kuwa, Simba ina 'warithi' kibao, hivyo pengo hilo kwa  sasa hakuna.

Lakini, hili tisa, Kocha msaidizi wa  Simba, Selemani Matola amesema, pamoja na ushindani  huo, lakini kuna kijana mmoja matata ambaye anaitendea haki nafasi ambayo Singano alikuwa anacheza, huyu ni Peter Mwalyanzi.

Matola ambaye ndiye kocha aliyewaibua wachezaji  wengi vijana akiwemo Ramadhani Singano, alimweleza mwandishi wa  habari  hizi akiwa katika mazoezi ya jana (juzi) yanayoendelea jijin kuwa, Mwalyanzi ni kati ya  wachezaji wanaoweza kucheza namba zote za winga, lakini ana kiwango cha kuaminika katika kikosi  cha msimu huu.

Kocha  huyo alisema, ujio wa Peter Mwalyanzi, Hamis Kiiza, Simon  Sserunkuma na Mussa Hassan Mgosi umeziba kabisa  pengo la  Messi,  na kukiri kuwa, ushindani wa  idara  ya ushambuliaji wa pembeni utakuwa mkubwa na kuliweka katika  wakati mgumu  benchi la  ufundi.

Alisema, tangu  Simba ilipanza kambi ya majuma mawili mjini Lushoto amebaini ugumu wa nani apangwe na yupi wa kusubiri kati ya Mwalyanzi (Peter) Hamis Kiiza, Simon Sserunkuma na Mgosi ambao  wote wanamudu kucheza kama winga.

Aliongeza kuwa, licha ya  ushindani  uliopo, wachezaji  wote hao ni mafundi wa  kucheza zaidi ya nafasi mbili uwanjani, hatua ambayo inawapa makocha ugumu wa kupanga kikosi cha kwanza.

"Mwalyanzi ana uwezo mkubwa wa kucheza kama winga wa kushoto, lakini ni fundi pia akipangwa kama kiungo mshambuliaji".

"Kiiza (Hamis) Mgosi na Simon (Sserunkuma) nao wapo katika  kiwango kizuri kucheza kama winga na hata washambuliaji, hapo ndipo unapoona kazi ya kupanga kikosi itakavyokuwa ngumu zaidi msimu huu" alisema Matola.

Matola  alisema, mfumo wa  sasa wa kocha Dylan Kerr  unamtaka kila mchezaji kuwa na uwezo wa kucheza katika nafasi mbili na kwamba  kila mchezaji wa kikosi cha msimu ujao anamudu vigezo na masharti.

Katika mazozi ya kila  siku   yanayoendelea  visiwani hapa (Unguja) kocha Kerr amekuwa akiwapanga wachezaji katika idara tofauti na kila  mmoja alionesha kumudu kwenda na mfumo autakao mzungu  huyu.

No comments:

Post a Comment