Sunday, August 30, 2015

Ndayisenga akubali kutua Simba


SIMBA SC imefikia makubaliano na wakala Dennis Kadito kuhusu mshambuliaji Mrundi, Kevin Ndayisenga na sasa mchezaji huyo anakuja kusaini timu ya Msimbazi.

Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Simba SC, Zacharia Hans Poppe amesema kwamba Ndayisenga anarudi kusaini baada ya kumalizana na wakala wake, Kadito.

“Mazungumzo yetu ya awali na Kadito hayakufanikiwa kwa sababu kadha wa kadha. Lakini imekuwa bahati tumerudi mezani tena na tumefikia makubaliano, sasa Ndayisenga anarudi,”amesema Poppe.

Kuhusu washambuliaji wengie wawili wa majaribio, Makan Dembele wa Mali na Pape Abdoulaye N’daw wa Senegal, Poppe amesema atasajiliwa mmoja wao. “Na si lazima tusajili, tunaweza kuachana na wote iwapo hawataonyesha uwezo wa kuridhisha,”amesema.

N’daw jana alifanywa mtihani wa kwanza wa majaribio wakati Simba SC ilipomenyana na JKU Uwanja wa Amaan, Zanzibar, wakati Dembele alitarajiwa kutua jana .

N’daw anatokea klabu ya Dinamo Bucuresti ya Ligi Kuu ya Romania wakati Dembele anatokea JS Kabyle ya Algeria.

No comments:

Post a Comment