Tuesday, September 1, 2015

Chicharito apata timu mpya

Javier Hernandez 'Chicharito' kushoto akiwa katinga uzi wa klabu yake mpya (kulia) ni mgurugenzi wa michezo wa Bayer Leverkusen Rudi Voller
Javier Hernandez ‘Chicharito’ kushoto akiwa katinga uzi wa klabu yake mpya (kulia) ni mgurugenzi wa michezo wa Bayer Leverkusen Rudi Voller
Mshambuliajin wa Manchester Unitd, Javier Hernandez ‘Chicharito’ amehamia ligi ya Bundesliga kunako klabu ya Bayer Leverkusen kwa dau la pauni milioni 12. 
Chicharito ametua Ujerumani jana asubuhi akiwa ameruhusiwa kuondoka Old Trafford majira haya ya joto baada ya kushindwa kumshawishi kocha wa timu hiyo Lois van Gaal. 
Mshambuliaji huyo mwenye miaka 27 msimu uliopita aliutumia akiwa kwenye ligi ya La Liga akikipiga kwa miamba ya Hispania timu ya Real Madrid. Japo United inauhaba wa washambuliaji Chicharito bado hakuweza kupata nafasi kwenye kikosi hicho wakati timu yake ya zamani ikiangukia pua mbele ya Swansea Jumapili iliopita. 
Mchezaji huyo wa kimataifa wa Mexico amesaini mkataba wa miaka mitatu baada ya pande zote mbili kukubaliana ada ya pauni milioni 12. 
West Ham walikuwa wakivutiwa na Chicharito na walikuwa tayari kumsainisha mkataba lakini walishindwa kufanya hivyo kutokana na mchezaji huyo kuhitaji mshahara ambao West Ham waliona hawawezi kumudu kumlipa.

No comments:

Post a Comment