Saturday, August 15, 2015

HII NDIO TIMU ILIYOMDAKA KASEJA

kasejaMlinda mlango mkongwe nchini Juma Kaseja amesema kumekuwa na timu nyingi ambazo zimekuwa zikitaka kumsajili baada ya kupata ruhusa rasmi kutoka Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) kujiunga na timu yoyote itakayokuwa inahitaji huduma yake wakati akisubiri hatma ya kesi yake na klabu ya Yanga.
Golikipa huyo wa zamani wa timu ya Taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’ amevitaja baadhi ya vilabu ambavyo vimekuwa vikiiwinda saini yake kuwa ni Mbeya City, Ndanda FC pamoja na African Sports.
Habari za ndani zaidi zinasema kuwa, Kaseja tarari ameshamalizana na Coastal Union ya Tanga na amerejea jijini Dar es Salaam kuja kuchukua vitu vyake tayari kwa kuanza maisha mapya kwenye klabu ya ‘Wagosi wa Kaya’ kwa ajili ya msimu ujao.
Hapa chini unapata fursa ya kumsikiliza Kaseja akivitaja baadhi a vilabu vinavyopigana vikumbo kumsajili, bofya hapo kusikiliza stori kamili.

No comments:

Post a Comment