Friday, August 28, 2015

Everton yakataa ombi la John Stones kutua Chelsea


stonesssss
Licha ya klabu ya Everton kupelekewa ofa tatu na Chelsea za pauni milioni 20, 26m na 30 kwa ajili ya beki wao John Stones,pia beki huyo kupeleka barua ya kuomba kuondoa klabuni hapo, bado club ya everton imeendelea kukataa kumuuza mchezaji huyo.
Kupitia tovuti ya klabu hiyo mwenyekiti wa club hiyo Bill Kenwright amesema “club ya Everton imekataa ombi la John stones la kuhamia klabu nyingine, tangu kufunguliwa kwa dirisha la usajili tumekataa ofa mbalimbali kwa ajili ya John”.
Akamalizia kwa kusema “John sio wa kuuzwa na atabaki kua mchezaji wa muhimu katika timu yetu”.
Kocha wa Everton alipoulizwa kuhusu kukataliwa kwa ombi la John alisema “Bado hatujalikataa sababu leo ni siku ya mechi na suala la kuhama halikua kipaumbele chetu.Tutalikataa asubui na kuendelea na shughuli zetu.”

No comments:

Post a Comment