Thursday, August 13, 2015

STEWART HALL ASHINDA MECHI YA 11 MFULULZO TANGU AREJEE AZAM FC, YAILAZA 1-0 KMKM

 

REKODI YA STEWART HALL TANGU AREJEE AZAM FC JUNI 2015

Azam FC 4-2 Friends Rangers (Kirafiki Chamazi)
Azam FC 1-0 JKT Ruvu (Kirafiki Chamazi)
Azam FC 1-0 African Sports (Kirafiki Tanga
Azam FC 1-0 Coastal Union (Kirafiki Tanga)
Azam FC 1-0 KCCA (Kagame Taifa)
Azam FC 2-0 Malakia (Kagame Taifa)
Azam FC 5-0 Malakia (Kagame Taifa)
Azam FC 0-0 Yanga SC (pen5-3, Robo Fainali Kagame Dar)
Azam FC 1-0 KCCA (Nusu Fainali Kagame Dar)
Azam FC 2-0 Gor Mahia (Fainali Kagame)
Azam FC 1-0 KMKM (Kirafiki Zanzibar)
KOCHA Muingereza Stewart John Hall usiku huu ameiongoza Azam FC kushinda mechi ya 10 mfululizo tangu arejee kwa mara ya tatu Juni mwaka huu, baada ya kuifunga KMKM 1-0 Uwanja wa Amaan, Zanzibar.
Bao pekee la Azam FC katika mchezo wa leo limefungwa na beki Gardiel Michael Kamagi Mbaga kwa shuti la umbali wa mita 14 baada ya pasi ya Ramadhani Singano ‘Messi’.
Akiichezea kwa mara ya kwanza Azam FC tangu ahamie kutoka Simba SC mwezi uliopita, Messi alionyesha kiwango kizuri kuelekea mechi ya Ngao ya Jamii dhidi ya Yanga SC Agosti 22, Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Azam FC imeweka kambi Zanzibar kujiandaa na mchezo wa Ngao ya Jamii dhidi ya mabingwa wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, Yanga SC wiki ijayo. 
Wapinzani wao, Yanga SC wameweka kambi Tukuyu, Mbeya na leo pia walikuwa wana mchezo wa kirafiki, ambao wameshinda bao 1-0 dhidi ya Tanzania Prisons Uwanja wa Sokoine, Mbeya.

No comments:

Post a Comment