Thursday, August 27, 2015

Kerr afumua kikosi cha Ligi Kuu


WAKATI ambapo Ligi Kuu ya msimu huu inatarajia kuanza kutimua vumbi Septemba 12 mwaka huu, Kocha Mkuu wa Wekundu hao amepangua kikosi na kukipanga upya kwa mfumo wa 4:3:3 ambao umezaa matunda katika mechi za kirafiki.

Mfumo huo unatokana na matokeo ya mechi zote za kirafiki ambazo Simba imeshacheza, ambao kocha Kerr ameanza kupata mwelekeo wa kupata kikosi chake cha kwanza.

Ingawa ni mapema mno, lakini mwenendo mzima wa mazoezi ya hivi karibuni inaonesha namna mzungu huyo anavyoanza maandalizi ya kupata kikosi cha kwanza, huku akiwaamisha namba baadhi ya wanandinga wake.

Katika mazoezi ya jana na juzi katika uwanja wa Amaan, Unguja, Kerr ameanza kuwahamisha idara baadhi ya wachezaji, ikiwa ni baada ya kubaini majukumu yao dimbani.

Hatua ya awali ya kocha Kerr imeanza kwa kuangalia mfumo wa wachezaji wa idara ya ulinzi kwa kuwapanga Juuko Murshid acheze na Hassan Isihaka, Mohamed Hussein 'Tshabalala' Abdi Banda, hivyo ni sawa na kuwahakikishia namba katika kikosi cha kwanza.

Katika idara ya kiungo, kocha huyo mzungu amewapa shavu kubwa Mwinyi Kazimoto, Justice Machabvi, Said Ndemla kuimarisha mfumo wa kuchezesha wachezaji watatu katika idara hiyo.

Mfumo wa kocha huyo umewapa nafasi wachezaji watatu katika safu ya kupanga mashambulizi kwa kuwapanga Peter Mwalyanzi, Mussa Hassan Mgosi na Ibrahim Ajibu na kuanzisha mfumo wa kuwa na washambuliaji watatu mbele.

Mfumo wa ambao kocha Kerr ameupanga ni kuchezesha mfumo wa 4:3:3 ambao umeanza kuzaa matunda katika mechi zote za kirafiki zilizochezwa na wanamsimbazi hao.

Kazi nyingine ilikuwa ni kupampanisha idara ya ulinzi na kiungo ambapo wachezaji Peter Mwalyanzi, Jonas Mkude,Said Ndemla, Simon Sserunkuma kwa mara nyingine wamepewa mbinu za kushuka hadi idara ya ulinzi na kupokea mipira na kupasiana haraka haraka huku wakikimbia kuelekea mbele.

Mfumo huu umewakosha makocha Dylan Kerr na Seleman Matola kwa wachezaji wote wa idara ya kiungo kuonyesha uwezo wa kucheza katika mfumo elekezi.

Akinukuliwa, kocha Kerr ameridhishwa na namna ambavyo mfumo wa 4:3:3 unavyoanza kuzoeleka na wachezaji, lakini akasisitiza kuwa fomesheni hiyo itategemea na aina ya timu npinzani watakayokutana nayo

"Tunaangalia uwezo wa kila mchezaji kabla ya kujenga kikosi.Tutaka kuona kila mchezaji anatekeleza jukumu lake na kutoa msaada kwa mwenzake wakati wote awapo mazoezini"

"Hii ndiyo ilikuwa kazi ya kipindi hiki cha mwisho cha kuandaa kikosi kabla ya kuanza kwa Ligi Kuu" alisema Kerr.

No comments:

Post a Comment