Thursday, August 27, 2015

Ivo Mapunda: Sikuikacha Simba, nimeachwa


IVO Mapunda
KIPA aliyeisaidia sana Simba kupata walau mafanikio iliyoyapata kwenye msimu uliopita, Ivo Mapunda ameagana rasmi na Simba, lakini akasisitiza kwamba hajaikacha Simba kama inavyoripotiwa, ila Simba waliamua kumtema.

Mapunda, amesema anarejea Kenya, baada ya kuachwa na klabu hiyo mapema mwezi huu, na kwamba usahihi ni kwamba Simba imemuacha sio kweli kwamba hakuwa tayari kuidakia Simba kama inavyotangazwa.

Ivo aliyewahi kudakia pia Yanga SC, amesema hana kinyongo na Simba SC na anaondoka nafsi yake ikiwa safi kwenda kutafuta maisha sehemu nyingine.

“Nawashukuru mashabiki wa mpira haswa wa Simba kwa kuwa nami kipindi chote, nilipofanya vibaya na nilipowaudhi mlikuwa nami na ndiyo soka ipo hivyo,”amesema.

Ivo Ameongeza; “Maisha yana changamoto na ndiyo nimezipata kwa sasa Simba baada ya watu fulani kufanya hivyo, ila naamini maisha ni popote na Mungu ndiye kila kitu,”.

Ivo amesema kwamba anarudi Kenya ambako bado anakubalika na anaamini atapata timu.

Ivo alijiunga na Simba SC Desemba 2013 akitokea Gor Mahia ya Kenya katika cha mwaka mmoja na nusu wa klabu hiyo ya Msimbazi, ameidakia jumla ya mechi 39 na kufungwa mabao 25, akiiwezesha timu hiyo

Zaidi Ivo aliwafurahisha mno wana Simba kwa kulinda vyema lango kwenye mechi dhidi ya mahasimu, Yanga SC na kwa kipindi chake chote Wekundu wa Msimbazi hawajapoteza mechi dhidi ya watani wao hao.

Alianza na mechi ya Nani Mtani Jembe mwaka juzi, Simba ikishinda 3-1, akadaka mechi ya Ligi Kuu, timu hizo zikitoka sare ya 1-1 kabla ya Desemba mwaka jana kuiongoza tena timu hiyo kushinda mechi ya Nani Jembe 2 mabao 2-0 na mechi yake ya mwisho ya watani kudaka, Wekundu wa Msimbazi walishinda 1-0 katika Ligi Kuu.

No comments:

Post a Comment