Thursday, August 27, 2015

Msenegal mpya aweka historia


Pape Abdoulaye N'Daw
KLABU ya soka ya Simba imeonesha jeuri moja kubwa. Imeachana na senegal Papa Niang. Lakini mara moja imemwita kundini msenegali mpya Pape Abdoulaye N'Daw.

N'Daw mwenye umri wa miaka 21, ametua jijini tayari kwa kuanza safari ya majaribio kabla ya kuliridhisha benchi la ufundi la kocha Dylan Kerr ambaye anahaha kupata mfumania nyavu wa kiwango cha juu.

Kwa mujibu wa taarifa mbalimbali, straika huyo kinda ana histori ambayo kama itakwenda sawa na kiwango katika majaribio bila shaka itampa ulaji katika kikosi cha Simba cha msimu huu.

Msenegal huyo kwanza ana historia ya kufunga mabao kadri anapopangwa na alifanya hivyo akiwa katika FC Dinamo Bucuresti ya nchini Romania.

Akiwa na timu hiyo,N'Daw alipachika mabao saba katika mechi 11 alizopangwa, ikiwa ni wastani nzuri zaidi kuwekwa na wachezaji kinda wa mfano wake.

Lakini, hadi anavyotua jijini Dar es Salaam, msenegali huyo ameacha historia ya kuipachikia timu yake ya sasa ya Ligi Kuu ya Niary Tally ya nchini Senegal, straika huyo amepachika mabao matano katika mechi nane alizopangwa.

Kwa mujibu wa historia hii inamweka straika huyo katika nafasi kubwa ya kufuzu majaribio, kwasababu kitakwimu inaonesha kuwa anakidhi haja na vigezo vya mahitaji ya kocha Dylan Kerr.

Kocha Dylan Kerr amekuwa akiwahimiza viongozi wa klabu hiyo kupata straika wa maana wa kuiwezesha Simba kuwa na safu hatari ya kuipa ushindi timu katika mechi za Ligi Kuu inayotarajia kuanza kutimua vumbi mwezi Septemba mwaka huu.

Awali,uongozi wa klabu ya Simba ilijipanga kumshusha kikosini straika Laudit Mavugo ambaye aliingia katika historia ya uwezo wa kupachika mabao katika ligi ya nchini Burundi, akiwa na timu yake ya Vital'0'.

Simba iliacha mpango wa kumwania Mavugo kutokana na dau ambalo Vital'0' ilikuwa ikihitaji la dola 11,000,000 ambalo sawa na shilingi 22 milioni, dau ambalo Wekundu wa Msimbazi waliona ni kubwa kwasababu awali hawakuambiwa kima hicho.

Kisha, Simba ilimgeukia mpachika mabao mwingine raia wa Burundi, Kelvin Ndayisenga ambaye hata hivyo kabla ya kuendelea na majaribio klabu yake na wakala walitaja dau la dola 70,000 ambalo ni sawa na takriban shilingi 140 milioni, hivyo wakaamua kuachana naye.

No comments:

Post a Comment