Wednesday, August 12, 2015

MGOSI ATIA AFANYA KWELI NDONDO CUP, FARU JEURI IKIICHAPA STAKISHARI

Mussa Hassan Mgosi (kushoto) akichuana na beki wa Stakishari FC
Mussa Hassan Mgosi (kushoto) akichuana na beki wa Stakishari FC
Goli la Mussa Hassan Mgosi na Salumu Gandi limeipa Faru Jeuri ushindi wa goli 2-0 dhidi ya Stakishari FC kwenye mchezo Ndondo Cup Sports Xtra chini ya udhamini wa Dr. Mwaka pamoja na Azam Food Products  ikiwa ni hatua ya 16 bora ya michuano hiyo mechi iliyochezwa kwenye uwanja wa Bandari, Tandika-Temeke, Dar es Salaam.
Mgosi Ndondo 5Mgosi alifunga goli hilo kipindi cha kwanza baada ya Faru Jeuri kutawala sehemu kubwa ya mchezo huo kwa kipindi cha kwanza na kufanikiwa kupata goli la kwanza dakika za mapema za kipindi cha kwanza. Hadi mapumziko Faru Jeuri walikuwa mbele kwa goli hilo la Mgosi.
Shaffih Dauda (katikati) akiwa na wadau wengine wa soka wakifuatilia pambano kati ya Faru Jeuri na Stakishari kwenye uwanja wa Bandari Tandika
Shaffih Dauda (katikati) akiwa na wadau wengine wa soka wakifuatilia pambano kati ya Faru Jeuri na Stakishari kwenye uwanja wa Bandari Tandika
Kipindi cha pili kilibadilika ambapo Stakishari walianza kuliandama lango la Faru Jeuri lakini juhudi zao zote hazikufanikiwa kuzaa matunda kutokana na ukuta wa Faru Jeuri kuwa mgumu kupitika.
Kikundi cha ushangiliaji cha timu ya Faru Jeuri kikishangilia baada ya Mgosi kuifungia timu yao goli la kwanza
Kikundi cha ushangiliaji cha timu ya Faru Jeuri kikishangilia baada ya Mgosi kuifungia timu yao goli la kwanza
Wakati Stakishari wakipambana kusawazisha goli, Faru Jeuri waliandika goli la pili dakika za lala salama kupitia kwa Salumu Gandi na kuipa Faru Jeuri ushindi wa goli 2-0 mbele ya Stakishari FC na kukata tiketi ya kusonga mbele katika hatua inayofuta ya michuano hiyo.
Wadau wa soka waliofurika kwenye uwanja wa  Bandari Tandika kushuhudia pambano kati ya Faru Jeuri dhidi ya Stakishari FC
Wadau wa soka waliofurika kwenye uwanja wa Bandari Tandika kushuhudia pambano kati ya Faru Jeuri dhidi ya Stakishari FC
Michuano hiyo itaendelea tena kesho (Jumatano) Agosti 12 kwa mchezo mmoja  ambao utawakutanisha Keko Furniture dhidi ya Buguruni United mchezo utakaopigwa kwenye uwanja wa Bandari Tandika-Temeke.

No comments:

Post a Comment