Sunday, August 30, 2015

Kiongera mambo saafi Msimbazi


PAUL Kongera
KAMA kuna anayedhani Wekundu wa Msimbazi hawana mpango na Paul Kiongera, hiyo itakuwa imekula kwake! Kwa taarifa yako tu, Straika huyo raia wa Kenya bado ni mali halali ya klabu ya Simba.

Lakini siyo hilo tu, kinachotakiwa kujulikana hapa ni kwamba, klabu ya Simba imepanga kumjumuisha kikosini ifikapo mwezi Desemba mwaka huu.

Haya yamebainishwa na Rais wa klabu ya Wekundu hao,Evans Aveva alipolitolea ufafanuzi suala la mpachika mabao huyo ambaye kwa sasa anacheza kwa mkopo katika tmu ya KBC inayoshiriki Ligi Kuu nchini Kenya.

Akiweka bayana, Aveva alisema, Kiongera bado ana mkataba na Simba na ndiyo maana ililazimika kumtoa kwa mkopo kwa timu hiyo ya Kenya.

Aveva alilazimika kutoa ufafanuzi suala la straika huyo baada ya kuwapo kwa ushauri wa wanasimba wanaoutaka uongozi kumrejesha kikosini mchezaj huyo katika kipindi hiki ambacho kocha Dylan Kerr anahaha kupata mfumania nyavu wa maana.

Akijibu, Aveva alisema, straika huyo ni mali yao na kwamba mwezi Desemba atarejea Msimbazi kama mchezaji halali na kuendelea na kandarasi ya kuitumikia klabu.

"Kiongera bado ni mchezaji wetu halali, tulimtoa kwa mkopo KBC kwa makubaliano maalum, hivyo lazima tuyaheshimu na kandarasi yake ya kucheza kwa mkopo itakoma mwezi Desemba mwaka huu" amenukuliwa rais huyo wa Simba.

Kiongera alisajiliwa na Simba msimu uliopita, lakini bahati mbaya hakudumu baada ya kuandamwa na majeraha mwanzoni kabisa mwa msimu alipoumia katika mchezo wa ufunguzi dhidi ya Coastal Union, uliomalizika kwa sare ya mabao 2-2.

No comments:

Post a Comment