Wednesday, August 12, 2015

Courtois nje ya mtanange wa Man City

Thibaut akipewa kadi nyekundu
Mlinda mlango wa klabu ya Chelsea ya nchini Uingereza Thibaut Courtois ataukosa mtanange dhidi ya Manchester City baada ya rufaa yake dhidi ya kadi nyekundu alioipata katika sare ya 2-2 dhidi ya Swansea kukataliwa.
Mlinda mlango huyo wa kimataifa wa Ubelgiji mwenye miaka 23, alitolewa nje alipomzuia mshambuliaji wa Swansea Bafetimbi Gomis nafasi ya kufumania nyavu katika mchezo uliopigwa jumapili darajani Stamford.
Chama cha soka cha uingereza FA, kimesema Chelsea imeshindwa kuthibitisha kuwa mwamuzi Michael Oliver alifanya makosa katika mchezo huo.pamoja na hayo Asmir Begovic aliyesajiliwa katika majira ya kiangazi kutoka Stoke City anatarajiwa kusimama langoni dhidi ya City.
Chelsea mabingwa watetezi wa ligi kuu ya Uingereza wanatarajiwa kuwakabili Man City walioshika nafasi ya pili msimu uliopita jumapili hii katika uwanja wa Ethihad.

No comments:

Post a Comment