Wednesday, September 23, 2015

Malinzi aota kombe la Dunia

Jamal Malinzi, Rais wa TFF
Jamal Malinzi, Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)
Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu (TFF) Jamal Malinzi ameendelea kusisitiza kwamba Tanzania itashiriki michuano ya kombe la dunia miaka ijayo kutokana na maandalizi ambayo tayari yameanza kufanywa na shirikisho hilo kwa kuanza kujenga timu za vijana.
Pia katika hilo Malinzi ameongeza kwamba, tayari wameshaomba na kukubaliwa kuandaa michuano ya mataifa ya Afrika kwa vijana wa U17 michuano inayotarajiwa kufanyika mwaka 2019 huku akisisitiza tayari timu kwa ajili ya kushiriki michuano hiyo imeshaanza kuanaliwa.
Malinzi ametoa kauli hiyo leo wakati akifunga kozi ya makocha wa leseni C ya CAF iliyokuwa ikifundishwa na Salum Madadi ambaye ni mkurugenzi wa ufundi wa TFF.
“Sisi kama TFF tumesema kwamba mwaka 2020 tutacheza fainali za Olympic za Tokyo tumesema hivyo na tunaomba Mungu atusaidie”, amesema Malinzi.
“Kama tukiweza kufanikiwa 2020, tukacheza fainali za Olympic Tokyo, 2026 tutakuwa na timu ya na timu ya kucheza kombe la dunia mwaka 2026”.

No comments:

Post a Comment