Wednesday, September 16, 2015

Nsa Jobu aikimbia African Sports, uongozi wafafanua

Nsa Jobu, Mshambuliaji wa zamani wa klabu za Coastal Union na Villa Squad

Uongozi wa timu ya African Sports ‘wanakimanumanu’ umekiri kuwepo kwa hali ya sintofahamu baada ya kukimbiwa na mchezaji wake Nsa Jobu aliyesajiliwa kukisaidia kikosi hicho kilichopanda daraja kucheza ligi kuu Tanzania bara msimu huu.
Katibu mkuu wa kikosi hicho Khatibu Enzi amesema mchezaji huyo ametoweka kwenye kambi ya timu hiyo bila taarifa yoyote.
“Ni kweli Nsa Jobu mpaka dakika hii taarifa zake zinakwenda tofauti kwa sababu mara ya kwanza tulipata mawasasiliano kwamba amepatwa na msiba, lakini mpaka sasa mawasiliano yanakwenda tofauti kwahiyo bado sijapata jibu la kuweza kumjibia”, amesema Enzi.
“Kwa mara ya mwisho tumewasiliana wiki moja iliyopita akatuelezea dharura zake na tukamfanikishia, lakini kwa siku za hivi karibuni amekuwa hapatikani. Suala lake tumeliweka pembeni kidogo sasahivi tunaangalia mambo ya mechi dhidi ya Mwadui”.
“Tuna mkatabanae wa mwaka mmoja, hilo ni suala la klabu tunaweza kufanya marekebisho, kwasababu mikataba ipo basi tutalifanyia kazi”.
Timu hizo zinakutana Septemba 17 (Alhamisi) kwenye mchezo wao wa raundi ya pili huku timu zote zikiwa zimechezea vichapo kwenye mechi zao za kwanza, African Sports walibanwa na Myama Simba kwenye uwanja wa Mkwakwani wakati Mwadui FC wao walikula kibano kutoaka kwa Toto Africans kwenye uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza.

No comments:

Post a Comment