Wednesday, September 16, 2015

Minziro: Nitafanya vizuri kwenye Ligi Kuu msimu huu

minziro-e1415273563704 
Kivumbi cha ligi kuu ya kandanda Tanzania bara kikiwa kimeanza, kikosi cha maafande wa JKT Ruvu kimeshawasili jijini Mbeya tayari kwa mchezo wao wa kuwania taji la ligi hiyo mchezo utakaopigwa siku ya Jumatano kwenye uwanja wa kumbukumbu ya Sokoine.
Mtandao huu umezungumza na kocha wa maafande hao Fred Felix Minziro kutaka kujua mikakati ya kikosi chake kulekea mchezo huo mara baada ya kuchezea kichapo kwenye mchezo wa kwanza mbele ya Majimaji ya Songea.
“Kwaujumla game haikuwa nzuri kwetu na performance haikuwa kama tulivyotarajia kwahiyo ni vitu ambavyo nimejaribu kuvifanyia masahihisho pamoja na mambo mengine madogomadogo basi naamini Mungu akijalia mechi itakuwa nzuri Jumatano”, amesema Minziro.
“Bado ninakikosi bora na imara na naamini nitafanya vizuri kwenye msimu huu wa ligi”.
“Hakuna asiyejua kwamba Mbeya City ni wazuri, mechi itakuwa ni yenye ushindani kutokana na Mbeya City nao walivyofanya usajili na kuwa na kikosi imara”.
Mechi hii inatarajiwa kuwa ni moja kati ya mechi zitakazokuwa ngumu na ushindani mkubwa kutokana na timu zote kupoteza mechi zao za kwanza msimu huu. Mbeya City wao walipoteza mhezo wao wa kwanza wakiwa kwenye uwanja wao wa nyumbani mbele ya Kagera Sugar wakati JKT Ruvu wao walifungwa mchezo wao wa kwanza na Majimaji ya Songea kwenye uwanja wa Majimaji mjini Songea.

No comments:

Post a Comment