Wednesday, September 30, 2015

Timu Ligi daraja la kwanza yabadilisha wachezaji wanne mechi moja

Friends Rangers 1 
Katika hali isiyokuwa ya kawaida, kumeshuhudiwa tukio la kushangaza kwenye soka la Tanzania baada ya timu ya KMC ya Kinondoni  inayoshiriki ligi daraja la kwanza (FDL) kufanya mabadiliko kwa kuwaingiza wachezaji wanne kitu ambacho ni kinyume cha utaratibu wa soka.
Tukio hilo lilitokea tarehe 27.9.2015 wakati KMC ikicheza dhidi ya Friends Rangers kwenye uwanja wa Karume ambapo KMC ilifanya mabadiliko kwa kuwaingiza Frank Mashoto badala ya Kudra Omari, Kamongo Morris badala ya Mrisho Simon, Mfanyeje Musa badala ya Kabange Mgunda na Sultani Kasiras badala ya Adam Said.
Mechi hiyo namba 8 ya Kundi A ilimalizika kwa KMC kuibuka na ushindi wa goli 2-1 dhidi ya Friends Rangers.
Baadae Friend Rangers ilikata rufaa juu ya ushindi huo wa KMC kwasababu walikiuka kanuni na 14 (25) na maamuzi yaliyotolewa na TFF tarehe 30.9.2015 yameipa ushindi timu ya Friend Rangers huku KMC ikipigwa faini ya Tsh 200,000/=. Mwamuzi wa akiba anafutwa kuchezesha ligi msimu huu na mwamuzi wa kati anapewa onyo.
IMG-20150929-WA0002
IMG-20150929-WA0001

No comments:

Post a Comment