Tuesday, September 1, 2015

Hizi ndio sababu zilizokwamisha De Gea kuhamia Real Madrid

de Gea asalia 
David de Gea ameachwa njia panda asubuhi ya leo baada ya kusubiri kwa muda mrefu kuhama kutoka Manchester United kwenda Real Madrid kufuatia baadhi ya ‘documents’ kushindwa kufika kwenye makao makuu ya bodi ya usajili ya Hispania wakati vilabu hivyo vikijaribu kufanya uhamisho wa mlinda mlango huyo usiku wa manane hadi dirisha la usajili kufungwa nchini Hispania.
De Gea alikuwa akiamni kwamba, ndoto zake zimetimia za kuhamia Madrid kufuatia miamba hiyo ya La Liga kuvunja ukimya na kuikatia Man U kitita cha pauni milioni 29 jana (Jumatatu) mchana. Golikipa wa Madrid Keylor Navas pia alikuwa sehemu ya dili hilo ambapo angejiunga na Manchester kama sehemu ya usajilin wa De Gea.
Chanzo kutoka Real Madri kinasema kwamba, Madrid wanailaumu Manchester United kwa kushindwa kutuma doments sahihi kwenda LFP shirikisho la soka la Hispania jana usiku.United wamekanusha madai hayo wakisema kuwa, walipata uhakika kuwa document zao zimetumwa kwa wakati muafaka unaotambuliwa na FIFA. 
Uongozi wa LFP unasema United walizijaza document hizo kwa mfumo ambao mtu mwingine asingeweza kuzifungua.  
Klabu zote zinataka dili hilo likamilishwe na zinatarajia leo (Jumanne) kukata rufaa kwenye shirikisho la soka duniani FIFA.

No comments:

Post a Comment