Wednesday, September 23, 2015

Gabriel ashinda kesi, lakini bado majanga

Gabriel 
Mlinzi wa Arsenal Gabriel ameshinda rufaa yake baada ya klabu yake kupeleka ushahidi wa picha za video kumtetea mlinzi huyo.
Mwamuzi Mike Dean aliyechezesha mchezo kati ya Chelsea dhidi ya Arsenal Jumapili iliyopita, alimtoa nje kwa kadi nyekundu beki huyo raia wa Brazil akidaiwa kumganyaga kwa nyuma mshambuliaji wa Chelsea Diego Costa lakini picha za video zilizopelekwa kama ushahidi kwenye chama cha soka cha England (FA) hazioneshi kama Costa aliguswa na mguu wa Gabriel.
Chama cha soka nchini England kiliendelea kusubiri hadi saa 12 jioni siku ya Jumanne kuona kama Costa atawasilisha rufaa yake lakini haikuwa hivyo na kupitisha adhabu ya kumfungia mechi tatu.
Kocha wa Chelsea Jose Mourinho tayari ameshaamua kumtumia Radamel Falcao kwenye mechi dhidi ya Walsall siku ya Jumatano kwenye mchezo wa kombe la Capital One.
Lakini wakati huohuo, Gabriel bado anakabiliwa na kesi ya utovu wa nidhamu aliounesha mara baada ya kuoneshwa kadi nyekundu na Mike Dean huku akionekana kutaka kugoma kutoka nje ya uwanja.
Lakini maamuzi hayo yanamaanisha Gabriel atacheza mchezo wa Capita One siku ya Jumatano dhidi ya Tottenham.

No comments:

Post a Comment