Wednesday, September 9, 2015

Kompany amchezea rafu binti yake

Vicent Kompany 
Kuna tabia fulani ambazo humfanya Vincent Kompany kuwa moja ya mabeki wenye mioyo iliyojaa hali ya ushindani muda wote katika ligi kuu nchini Uingereza.
Mbelgiji huyo si tu kana kwamba yuko ngangari kwa muonekano bali tu, bali pia ni mkatili na mshindani pindi awapo uwanjani. Amezaliwa na chembechembe za ushindi ndani ya moyo wake ambapo wakati wote anaweza kufanya chochote ili mradi tu timu yake ipate matokeo.
Kwa nini yanasemwa maneno hayo, ni kutokana na kile alichokifanya kwa binti yake mwenye umri wa miaka mitano (5) anayejulikana kwa jina la Sienna. Kompany alionekana akimkimbiza mwanae na wakati alipotaka kujifanya mjanja wa kukimbia, alimkwatua kidogo na kumuangusha chini bila ya kumletea maumivu yoyote yale.

No comments:

Post a Comment