Wednesday, September 23, 2015

Ferguson awataja wachezaji wanne bora kuwahi kuwafundisha

Man utd 4 
Kocha mstaafu wa Manchester United Sir Alex Ferguson katika kitabu chake kipya cha hivi sasa, amewataja wachezaji wanne wa kiwango cha dunia kuwahi kuwafundisha.
Alex Ferguson amemtaja Cristiano Ronaldo kuwa ndiye mchezaji bora zaidi kuwahi kumfundisha huku akiwaongeza Erick Cantona, Ryan Giggs na Paul Scholes kama wachezaji wake bora wa kiwango cha dunia.
Man utd 42 
Alex anasema, “katika kitabu changu kuna wachezaji wawili tu wa kiwango cha dunia ambao bado wanacheza hadi sasa, Ronaldo na Messi”.
Man utd 41 
Katika orodha hiyo hakuna majina ya wachezaji Wayne Rooney, David Beckham wala Rio Ferdinand.
Lakini Fergie anasema aliowataja, wamethibitisha ubora wao huku akimwagia sifa Ryan Giggs kwamba atakuja kuwa ni kocha mkubwa na mafanikio mengi siku moja.
Akiongea kuhusu kitu anachokijutia katika maisha yake ya ukocha, Fergie anasema ni kutokushinda mataji mengi ya Ulaya ingawa alishinda makombe mbalimbali ya nyumbani.
Man utd 43

No comments:

Post a Comment