Wednesday, September 16, 2015

Timu ya Ngassa Afrika Kusini mambo poa

Ngasa Sauz 
Baada ya kuanza kwa vipigo vitatu mfululizo katika ligi kuu soka nchini Afrika Kusini, klabu ya soka ya Free States Stars FC anayoichezea mtanzania Mrisho Ngassa sasa imeibuka katika mechi yake ya nne na kupata ushindi mnono.
Free States Stars Fc ikicheza kwa uhakika zaidi katika uwanja wake wa nyumbani, imewalaza Chipa United kwa jumla ya magoli 3-0 na kukusanya points tatu muhimu kwa mara ya kwanza tangu kuanza kwa msimu.
Ushindi huo umekuja mara baada ya klabu ya Free States Stars kumfungisha virago aliyekua kocha wao na kumpa mkataba kocha mpya ambaye ameleta mabadiliko makubwa kiuchezaji kikosini.
Mtanzania Mrisho Ngassa ameendelea kutesa tu kutokana na kuendelea kuaminiwa na hata mwalimu mpya kwa kucheza katika dakika zote tisini akicheza nafasi ya kiungo mshambuliaji.
Magoli haya matatu yalifungwa na mshambuliaji raia wa Ubelgiji mara mbili Andre Filecia huku lingine likifungwa na mzawa Danny Venter.

No comments:

Post a Comment