Baada
ya kuanza kwa vipigo vitatu mfululizo katika ligi kuu soka nchini
Afrika Kusini, klabu ya soka ya Free States Stars FC anayoichezea
mtanzania Mrisho Ngassa sasa imeibuka katika mechi yake ya nne na kupata
ushindi mnono.
Free States Stars Fc ikicheza kwa
uhakika zaidi katika uwanja wake wa nyumbani, imewalaza Chipa United
kwa jumla ya magoli 3-0 na kukusanya points tatu muhimu kwa mara ya
kwanza tangu kuanza kwa msimu.
Ushindi huo umekuja mara baada ya
klabu ya Free States Stars kumfungisha virago aliyekua kocha wao na
kumpa mkataba kocha mpya ambaye ameleta mabadiliko makubwa kiuchezaji
kikosini.
Mtanzania Mrisho Ngassa
ameendelea kutesa tu kutokana na kuendelea kuaminiwa na hata mwalimu
mpya kwa kucheza katika dakika zote tisini akicheza nafasi ya kiungo
mshambuliaji.
Magoli haya matatu yalifungwa na
mshambuliaji raia wa Ubelgiji mara mbili Andre Filecia huku lingine
likifungwa na mzawa Danny Venter.
No comments:
Post a Comment