Friday, September 4, 2015

Simba yasajili 27 kwa msimu mpya Ligi Kuu


SIMBA SC imesajili wachezaji 27 kwa ajili ya msimu mpya wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara unaoanza wiki ijayo.
Katika orodha hiyo, Simba SC imekamilisha orodha ya wachezaji saba wa kigeni kwa kuwasajili Vincent De Paul Angban wa Ivory Coast, Emery Nimubona wa Burundi, Hamisi Kiiza, Simon Sserunkuma na Juuko Murushid wote wa Uganda, Justice Majabvi wa Zimbabwe na Pape Abdoulaye N’daw wa Senegal.
 Kutoka kulia, Justuce Majabvi, Awadh Juma na Nahodha Mussa Hassan Mgosi miongoni mwa wachezaji wa Simba SC waliosajiliwa kwa ajili ya msimu ujao  
 
KIKOSI KAMILI SIMBA SC;
Makipa; Vincent De Paul Angban, Peter Manyika
Denis Deonis Richard.
Mabeki; Mohamed Hussein, Hassan Ramadhani Kessy, Emery Nimubona, Samih Hajji Nuhu, Hassan Isihaka, Murushid Juuko, Mohamed Fakhi na Said Issa,
Viungo; Abdi Banda, Jonas Mkude, Justice Majabvi, Awadh Juma, Saidi Hamisi Ndemla, Mwinyi Kazimoto, Peter Mwalyanzi, Simon Serunkuma na Joseph Kimwaga.
Washambuliaji; Ibrahim Hajibu, Issa Abdallah, Daniel Lyanga, Boniphace Maganga, Hamisi Kizza, Pape Abdoulaye Ndaw na Nahodha Mussa Hasan Mgosi.

No comments:

Post a Comment