Mbio za kuwania ubingwa wa ligi
kuu Tanzania bara zimeendelea jana kwenye viwanja saba huku timu 14
zikipambana viwanjani kuwania pointi tatu muhimu kujiimarisha kwenye
msimamo wa ligi hiyo msimu huu.
Jijini Tanga wenyeji Mgambo JKT
walikuwa wakiwaalika ‘Wekundu wa Msimbazi’ Simba kwenye uwanja wa
Mkwakwani ambapo Simba wamechomoza na ushindi wa goli 2-0 magoli
yaliyofungwa na Justice Majabvi na Hamisi Kiiza.
Timu ya Majimaji ikiwa nyumbani
kwenye uwanja wa Majimaji mjini Songea imechomoza na ushindi wa goli 1-0
dhidi ya Kagera Sugar, pambano jingine lilikuwa ni kati ya Toto
Africans ‘wana kishamapanda’ ambao wao walikuwa nyumbani kwenye uwanja
wa CCM Kirumba kuikabili Mtibwa Sugar mchezo uliomalizika kwa Mtibwa
kutwaa pointi tatu kwa kuifunga Toto goli 2-0.
Kwenye dimba la Sokoine, timu ya
Mbeya City imeibuka na ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya maafande wa JKT
Ruvu. Azam wakiwa ugenini kwenye uwanja wa CCM Kambarage wamefanikiwa
kuitungua Stand United kwa goli 2-0 wakati Ndanda FC wakiwa nyumbani
kwenye dimba la Nangwanda Sijaona wameandika ushindi wa kwanza
wakiichapa Coastal Union kwa goli 1-0.
No comments:
Post a Comment