Tuesday, September 1, 2015

Ronaldo na Messi 'warogana'

Lionel-Messi-vs-Ronaldo-comparison 
Huwezi kutaja radha za kuangalia ligi kuu soka nchini Spain, La Liga bila kufuatilia ushindani wa magwiji wa soka hivi sasa ulimwenguni Cristiano Ronaldo na Lionel Messi.
Ushindani kati ya wawili hao umeleta hisia tofauti na mvuto wa aina yake katika ligi hiyo na kuongeza ladha ya pambano la El Classico ‘Real Madrid vs Fc Barcelona’ kutokana na mashabiki kutaka kuona ni mchezaji yupi ataisaidia timu yake kuibuka shujaa.
Hadi sasa zimechezwa mechi mbili kwenye ligi hiyo kwa kila timu, lakini hakuna yeyote kati ya wawili hao ambae tayari amefunga goli. Kitu hicho kimepelekea utani wa kusema kuna uchawi unaendelea baina ya miamba hao ambao huwa na kawaida ya kushindana kila mmoja akitaka kufunga zaidi ya mwenzake.
Ligi bado mbichi na wengi wanaamini siku Messi akifunga goli na upande wa pili utajibu mapigo, Ronaldo naye atafunga, tusubiri kuona hilo.
Wawili hao wamekua wakishindana kwa kila hali, idadi ya magoli, hat-trick pamoja na tuzo binafsi kama za Ulaya na dunia kwa ujumla kitu kilichoongeza utamu wa la liga katika miaka sita hivi sasa.

No comments:

Post a Comment