Wednesday, September 23, 2015

Ligi daraja la kwanza yadhaminiwa an Star Times

Mkurugenzi mkuu wa Star Times Llao Lan Fang (kuhoto) na Rais wa TFF Jamal Malinzi wakisaini mkataba wa udhamini wa ligi daraja la kwanza Tanzania bara
Mkurugenzi mkuu wa Star Times Liao Lan Fang (kuhoto) na Rais wa TFF Jamal Malinzi wakisaini mkataba wa udhamini wa ligi daraja la kwanza Tanzania bara
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) leo limesaini mkataba wa udhamini wa ligi daraja la kwanza (FDL) na kampuni ya Star Times Media wenye thamani ya shilingi milioni miatisa za kitanzania kwa muda wa miaka mitatu ili kusaidia gharama za uendeshaji wa ligi hiyo.
Utiaji saini huo umefanyika leo kwenye ukumbi wa Kisenga Millennium Towers, Makumbusho kati ya TFF na Star Times.
Llao Lang Fang akibadilishana mkataba na  Rais wa TFF Jamal Malinzi
Liao Lang Fang akibadilishana mkataba na Rais wa TFF Jamal Malinzi
Rais wa TFF Jamal Malinz ameishukuru Star Times kwa kukubali kudhamini ligi hiyo ili kuzisaidia timu shiriki  kujikimu pamoja na bodi ya ligi kuwalipa waamuzi pamoja na garama nyingine za uendeshaji wa ligi hiyo ambazo zimekuwa zikibebwa na TFF kwa miaka yote.
Malinzi amesema, kila timu itapata shilingi milioni 15. Milioni 10 kati ya hizo inatoka moja kwa moja Star Times wakati milioni tano itatoka kwenye haki za matangazo ya television kutokana na ligi hiyo kuonekana moja kwa moja (live) kupitia ving’amuzi vya Star Times.
Rais wa TFF Jamal Malinzi (kulia) pamoja na Mkurugenzi mkuu wa Star Times Media Llao Lan Fang wakionesha mkataba wa udhamini wa ligi daraja la kwanza Tanzania bara
Rais wa TFF Jamal Malinzi (kulia) pamoja na Mkurugenzi mkuu wa Star Times Media Liao Lan Fang wakionesha mkataba wa udhamini wa ligi daraja la kwanza Tanzania bara
Hata hivyo Malinzi amefafanua kuwa, mkata uliosainiwa leo ni wa udhamini wa ligi kutoka Star Times lakini wiki ijayo watasaini mkataba mwingine na kampuni nyingine itakayopewa haki ya kurusha matangazo ya mechi za ligi daraja la kwanza.
KUTOKA KUSHOTO: Mkurugenzi wa masoko Star Times Zuhura Hanif, Mkurugenzi mkuu Star Times Liao Lan Fang, Rais wa TFF Jamal Malinzi na Meneja masoko wa TFF Peter Simon
KUTOKA KUSHOTO: Mkurugenzi wa masoko Star Times Zuhura Hanif, Mkurugenzi mkuu Star Times Liao Lan Fang, Rais wa TFF Jamal Malinzi na Meneja masoko wa TFF Peter Simon
Liao Lan Fang ambaye ni mkurugenzi mkuu wa Star Times amesema, mbali na udhamini huo wa shilingi milioni miatisa, vilabu hivyo vitapta fursa ya kuonekana moja kwa moja kwenye nchi zaidi ya 10 za Afrika ambapo Star Times inapatikana.
Waandishi wa habari wakifanya kazi yao
Waandishi wa habari wakifanya kazi yao

No comments:

Post a Comment