Wednesday, September 9, 2015

Miguu ya Messi ni zaidi ya mikono yangu: Azarenka

Lionel Messi 5 
Nyota wa mchezo wa Tennis duniani Victoria Azarenka, amemimina pongezi kwa mchezaji mwenye kipaji cha ajabu ulimwenguni Lionel Messi, huku akisisitiza kwamba hucheza kama yupo kwenye ‘video game’ pindi awapo uwanjani.
Messi aliifungia Argentina mabao mawili katika ushindi wa mabao 7-0 dhidi ya Bolivia Jumamosi wiki ya iliyopita, japokuwa bado hajafunga katika michezo miwili ya ufunguzi wa La Liga kwa timu yake mpaka sasa.
Mbelarusi huyo mwenye umri wa miaka 26, ambaye amefika robo fainali ya michuano ya US Open na kutoa shukrani zake za dhati kwa mashabiki baada ya ushindi wake dhidi ya Varvara Lepchenko, amesema kuwa uwezo wa nyota huyo wa Barcelona ni kitu kama “kisichofikirika” na kuongeza kuwa mara nyingi humwangalia wakati akiwa mapumzikoni.
“Kumwangalia Messi akicheza ni kama vile unaangalia video game”, aliwaambai waandishi. “Ni kitu cha kusisimua sana”.
“Nisingeweza kuangalia mchezo ule kwa sababu ya tofauti ya masaa na kwa sababu siku hizi nina majukumu mengi kidogo, lakini ningeweza kumwangalia kwa sababu ya umaridadi wake”. 
“Anachokifanya Messi uwanjani ni kitu kisichoelezeka. Huwa najisikia furaha kubwa sana ninapomuangalia hasa akiwa na Barcelona na kusema tu ukweli, kwangu mimi, jamaa ni wa ajabu sana”. 
Azarenka alimalizia kwa kusema: “Wacheza soka hucheza kwa kutumia miguu. Siwezi kusema kwamba sidhani kama ubora wa mikono yangu katika Tennis ni kama yeye katika soka, lakini najaribu”.

No comments:

Post a Comment