Wednesday, October 21, 2015

Taarifa mpya kuhusu Nsa Job

Nsa Job, mchezaji wa zamani wa vilabu vya Simba , Yanga na Cosatal Union
Nsa Job, mchezaji wa zamani wa vilabu vya Simba , Yanga na Cosatal Union
Baada ya picha nyingi na taarifa kuzagaa zinazomhusu mchezaji wa zamani wa vilabu vya Yanga, Simba pamoja na Coastal Union Nsa Job akiwa amelazwa hospitali kufuatia kujeruhiwa vibaya na watu wanaodhaniwa kuwa ni wafuasi wa CHADEMA, imetoka taarifa kuwa hali yake inaendelea kuwa nzuri.
Mwenyekiti wa chama cha soka mkoa wa Kilimanjaro Goodluck Moshi amesema hali ya Nsa Job anaendelea vizuri akiwa bado amelazwa kwenye wodi ya wagonjwa mahututi lakini tayari ameondolewa mashine za kumsaidia kupumua.
“Taarifa iliyopo ni kwamba, alipigwa (Nsa Job) na jiwe kubwa kichwani wakati akiwa kwenye gari akitokea nyumbani kwa mgombea ubunge Manispaa ya Moshi kupitia Chama Cha Mapinduzi Ndugu Davis Mosha”, Moshi ametaarifu .
“Wakati wanatoka nyumbani kwa Mosha wakiwa kwenye gari yeye (Nsa Job), Mosha na mtu mwingine, walipofika barabarani, likarushwa jiwe kubwa likapita kwenye kioo cha dirisha na kumpasua kwenye kichwa na taya, akakimbizwa KCMC amefanyiwa upasuaji bado yupo ICU lakini hali yake inaendelea vizuri”.
“Ameshaondolewa mashine za kupumulia na anaweza kuongea hivi sasa, ni jambo la kumshukuru Mungu kutokana na hali halisi ilivyokuwa imejitokeza”.
Jana kuna picha zilienea kwenye mitandao ya kijamii zikionesha kuwa Nsa Job amelazwa kwenye wodi ya wagonjwa mahututi (ICU) baada ya kujeruhiwa vibaya kwenye eleo la kichwa.

No comments:

Post a Comment