Wednesday, October 28, 2015

Ratiba Ligi Kuu Tanzania Bara



Oktoba 28, 2015
Toto African Vs Mgambo Shooting
Mwadui FC Vs Yanga SC
Mtibwa Sugar Vs Kagera Sugar
Mbeya City Vs Majimaji FC
Ndanda FC Vs Stand United
Simba SC Vs Coastal Union
Oktoba 29, 2015
JKT Ruvu Vs Azam FC 
Prisons Vs African Sports

MCHEZAJI bora wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara mwezi Septemba, Hamisi Friday Kizza ‘Diego’ yuko tayari kurudi uwanjani leo.
Mganda huyo hajaonekana uwanjani tangu Simba SC ifungwe 2-0 na mahasimu, Yanga SC, Septemba 26, mwaka huu Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, lakini leo anaweza kurudi.
Simba SC inamenyana na Coastal Union ya Tanga katika mfululizo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara leo Uwanja wa Taifa na Ofisa Habari wa Simba SC, Hajji Sunday Manara amesema Kizza anaweza kurudi.
“Kama mchezaji yuko fiti na amefanya mazoezi kikamilifu kuelekea mchezo huu, sasa ni jukumu la kocha mwenyewe kumuanzisha au la. Maana kocha wetu (Muingereza Dylan Kerr) naye ana maamuzi yake,”amesema.
Mbali na Kizza, Manara amesema hata kiungo wao, Jonas Mkude naye yuko vizuri kabisa kuelekea mchezo wa leo na wanamuachia Kerr mwenyewe kama kawaida yake aamue wachezaji wa kutumia.
Kwa ujumla Manara amesema Simba SC haina mchezaji majeruhi wala mgonjwa kuelekea mchezo wa leo na wanasubiri kuona kocha Kerr atawapangia timu ya aina gani leo.
Kwa ujumla, Ligi Kuu inaendelea leo, mbali na Simba na Coastal- Mwadui FC inaikaribisha Yanga SC Uwanja wa Kambarage, Shinyanga, Toto Africans watakuwa wenyeji wa Mgambo Shooting Uwanja wa CCM Kirumba, Mwanza na Mtibwa Sugar watakuwa wenyeji wa ndugu zao Kagera Sugar Uwanja wa Manungu, Turiani, Morogoro. 
Mbeya City watakuwa wenyeji wa Majimaji FC Uwanja wa Sokoine, Ndanda FC wataikaribisha Stand United Uwanja wa Nangwanda, Mtwara wakati kesho JKT Ruvu watamenyana na Azam FC Uwanja wa Karume, Dar es Salaam na Prisons wataikaribisha African Sports Uwanja wa Mkwakwani, Tanga.

No comments:

Post a Comment