Wednesday, October 28, 2015

Rekodi zilizowekwa kwenye Ligi mbalimbali Ulaya mwishoni mwa wiki



MUNICH, Ujerumani
NCHINI Ujerumani, klabu ya Bayern Munich ilipata ushindi wake wa 1000 tangu kuanzishwa kwa ligi hiyo ya Bundesliga baada ya kuifunga FC Koln kwa mabao 4-0.
Katika mchezo huo, golikipa wa Bayern Munich, Manuel Neur aliweka rekodi ya kucheza mchezo wa 138 bila bila kuruhusu wavu wake kutikiswa.
Mchezaji mwingine wa klabu hiyo Arjen Roben aliweka rekodi ya kufunga bao lake la 75 katika ligi ya Bundesliga.
Mshambuliaji wa klabu ya Borussia Dortmund, Pierre Emerick amekuwa mchezaji pekee kutoka klabu ya Dortmund kufunga magoli 13 kwenye mechi 10 ndani ya ligi ya Bundesliga baada ya kufunga magoli matatu (hat-trick) katika ushindi wa Dortmund wa goli 5-1 ilipocheza dhidi ya FC Augsburg.

ITALIA
Klabu ya AS Roma imekwea kileleni mwa Serie A baada ya kupata ushindi wa magoli 2-0 na hiyo inakuwa mara ya kwanza kwa klabu hiyo kukaa kileleni tangu ilipofanya hivyo kwa mara ya mwisho kwenye msimu wa 2013-2014.
Kipa wa AC Milan, Gianluig Donnarumma ameweka rekodi ya kuwa kipa mdogo kucheza mchezo wa Serie A wakati timu yake ilipopata ushindi wa goli 2-1 dhidi ya Sousoro. Bonaroma alidaka kwenye mechi hiyo akiwa na umri wa miaka 16 miezi 8 na siku 6.

UFARANSA
PSG wameendeleza ushindi baada ya ushindi wa goli 4-1 dhidi ya ASSE na kuendelea kukaa kileleni mwa ligi ya Ufaransa.
Mpaka sasa PSG hawajapoteza hata mchezo mmoja kwenye ligi hiyo msimu huu huku timu hiyo ikiwa haijaungwa tangu mwezi Machi mwaka huu tangu walipofungwa na Bodeaux goli 3-2.
Klabu ya Olympic Marseille imepata ushindi wa kwanza kwenye Ligue 1baada ya michezo saba kufuatia ushindi dhidi ya klabu ya Lille wa goli 2-1.

HISPANIA
Baada ya kumshuhudia, Luis Suarez akifunga magoli matatu kwenye ushindi wa goli 3-1 dhidi ya Eibar, kocha wa Barcelona, Luis Enrique Martínez amesema hakuna wa kuziba nafasi ya Suarez hivi sasa.
Ilikuwa ni siku nzuri kwa Suarez kwani alikua akitimiza mwaka mmoja tangu acheze mchezo wake wa kwanza dhidi ya Real Madrid Oktoba 25 2014 katika uwanja wa Santiago Bernabeu.
Hiyo ilikuwa ni hat-trick ya pili kwa Suarez wakati hat-trick ya kwanza ilikuwa ni dhidi ya Cordoba katika ushindi wa Barcelona wa magoli 8-0 msimu uliopita.

ENGLAND
Jurgen Klopp alikuwa akiiongoza Liverpool kwenye mchezo wa kwanza wa ligi ya England katika uwanja wa Unfield dhidi ya Southampton, katika mchezo huo timu hizo zilitoka sare ya kufungana goli 1-1.
Liverpool imefunga magoli tisa tu msimu huu ikiwa timu ya tatu kwa kufunga magoli machache msimu huu ikizizidi klabu za West Brom na Watford pekee ambazo zimefunga magoli nane.
Klabu ya Sunderland imefunga maoli matatu kwa mara ya kwanza tangu tarehe 3 Novemba, 2014. Sunderland iliifunga Newcastle United kwa goli 3-0.
Goli la sekunde ya 49 lililofungwa na Matt Ritchie katika mchezo kati ya Bournemouth dhidi ya Tottenham linakuwa goli la mapema zaidi kwenye msimu wa ligi kuu England. Katika mchezo huo Bournemouth walifungwa goli 5-1 wakiwa kwenye uwanja wao wa nyumbani.
Harry Kane alifunga hat-trick yake ya pili kwenye Ligi Kuu England, alifanya hivyo dhidi ya Leicester City msimu uliopita.

No comments:

Post a Comment