Wednesday, October 21, 2015

Gharama za kiingilio chaikwamisha Wajerumani

Mashabiki wa Bayern Munich wakiwa wamebabeba mabango yenye ujumbe wa kupinga bei za viingilio vikubwa kwenye uwanja wa Emirates
Mashabiki wa Bayern Munich wakiwa wamebabeba mabango yenye ujumbe wa kupinga bei za viingilio vikubwa kwenye uwanja wa Emirates
Uwanja wa Emirates unaomilikiwa na Arsenal ndio unaoongoza kwa tozo kubwa ya viingilio vyake jijini London. Katika mchezo huo kati ya Arsenal na Bayern Munich, baadhi ya mashabiki wa Bayern walikataa kuingia uwanjani kutokana na bei kubwa za kiingilio.
Kikundi hicho cha mashabiki kutoka Ujerumani walikaa nje kwa dakika tano kabla ya kukubali kuingia uwanjani na kupata mapokezi makubwa kutoka kwa mashabiki wa Arsenal walipokua wakiketi katika seat zao.
Mashabiki hao waliingia na mabango waliyoyaandika, “tiketi paun 64?… Hakuna soka bila ya mashabiki”. Ujumbe huo uliandikwa kuonesha kutokukubaliana na gharama za uwanja huo.
Mashabiki wa Arsenal wakiwashangilia mashabiki wa Bayern Munich baada ya kukubali kuingia uwanjani kufuatia kugoma kwa dakika kadhaa
Mashabiki wa Arsenal wakiwashangilia mashabiki wa Bayern Munich baada ya kukubali kuingia uwanjani kufuatia kugoma kwa dakika kadhaa
Kocha wa Bayern Munich, Pep Guadiola alisema ataongea na Arsene Wenger siku nyingine wajaribu kuweka bei nafuu za viingilio kuwapa nafasi mashabiki wote kuingia uwanjani. Guadiola amesema kwa upande wake yeye Ujerumani atawajali mashabiki wa Arsenal na kuhakikisha wanapata viingilio rahisi washuhudie mechi.
Aidha katika mchezo wenyewe, Arsenal walifanikiwa kushinda kwa magoli 2-0 mbele ya Bayern Munich na kupata ushindi wa kwanza kabisa tangu kuanza kwa michuano hiyo ya Ulaya msimu huu.

No comments:

Post a Comment