Wednesday, October 28, 2015

Matokeo yote ya mechi za Capital One

Capital One Cup 1
Usiku wa Jumanne nchini England kulipingwa michezo minne ya kombe la Capital One, michezo mitatu kati ya minne iliamuliwa kwa changamoto ya mikwaju ya penati baada ya michezo yote mitatu kumalizika kwa sare ya kufungana goli 1-1.
Sheffield Wednesday wakapata ushindi wa goli 3-0 mbele ya Arsenal na kuing’oa Arsenal kwenye kombe la kwanza msimu huu.
Chelsea dhidi ya Stoke Cty mchezo uliopigwa kwenye uwanja wa Britania Stoke ikafanikiwa kuivua ubingwa Chelsea baada ya kuifunga kwa mikwaju ya penati 5-4 kufuatia sare ya kufungana goli 1-1. Walters aliifungia Stoke City goli la kuongoza dakika ya 52 lakini Loic Remy akaisawazishia Chelsea dakika ya 90.
Eden Hazard akakosa mkwaju wa penati wa mwisho baada ya dakika 120 za mchezo na kuhitimisha safari ya Chelsea kwenye michuano ya Capita One Cup.
Hull City waliwakaribisha Leicester City, Abel Hernandez aliifungia Hull City bao lakini  Riyad Mahrez akaifungia Leicester City bao la kusawazisha na kuufanya mchezo huo kuchezwa kwa dakika 120 na kumalizika kwa matokeo hayo ya kufungana bao 1-1.
Kwenye changamoto ya mikwaju ya penati, Hull City wakafanikiwa kusonga mbele baada ya Riyad Mahrez kukosa penati yake.
Kwenye uwanja wa Goodson Park Everton waliwakaribisha Norwich City mchezo uliomalizika kwa sare ya kufungana goli 1-1. Zikaongezwa dakika 30 lakini bado timu hizo hazikufuyngana, ikabidi itumike mikwaju ya penati kumpata mshindi na Everton wakafanikiwa kusonga mbele.
Capital One Cup results


No comments:

Post a Comment