Saturday, October 17, 2015

Martial kweli noma

Anthony Martial-tuzo 
Mshambuliaji wa klabu ya Manchester United Anthony Martial ametwaa tuzo ya mchezaji bora wa mwezi Septemba ikiwa ni tuzo ya kwanza kwa mchezaji wa Manchester United kwenye ligi kuu England chini ya kocha Louis van Gaal tangu ajiunge na klabu hiyo mwaka 2014.
Martial amecheza michezo minne kwenye ligi kuu ya England na tayari ameshafunga magoli matatu, Manchester United itacheza na Everton kwenye uwanja wa Goodson Park.
Kinda huyo wa Kifaransa alitua Old Trafford akitokea Monaco kwa ada ya uhamisho wa pauni 36 huku kukiwa na kipengele cha kuongezeka hadi pauni milioni 58.
Martia aliunga goli lake la kwanza dhidi ya Liverpool alipotokea benchi ambapo United iliibuka na ushindi wa goli 3-1. Mchezo kati ya Manchester United dhidi ya Southampton, Martial alifunga mgoli mawili wakati Manchester iliposhinda kwa goli 3-2.
Wakati Martial akichukua tuzo ya mchezaji bora wa mwezi Septemba, kocha wa Tottenham Mauricio Pochettino amechukua tuzo ya kocha bora wa mwezi wa tisa.

No comments:

Post a Comment