Wednesday, October 14, 2015

Arsenal yajipanga kumsajili kinda wa miaka 19


Riechedly Bazoer raia wa Holland ni moja kati ya wachezaji ambao wanaonekana kucheza vizuri sana, ukiangalia na umri wake basi ndio anazidi kuvutia wadau wa soka.
Arsenal wameshaonyesha nia ya kumsajili mchezaji huyu mwenye miaka 19 ambae kwa sasa anachezea club ya Ajax. Akiwa na miaka 16 alikataa kuhamia Arsenal ambapo Wenger alitaka kumsajili, baada ya miaka 3 ameonekana kuongeza kiwango chake na Wenger ameendeleza nia yake ya kutaka kumleta Arsenal. Kutakaa kwake kuhamia Arsenal alitaka uhakika wa kuendelea kucheza na kukua kimchezo akiwa nchini kwao Holland.
Uwezo wake na umri wake unazivutia club nyingi za Ulaya lakini Arsenal ndio inaonekana kuwa mbele kupata sign yake na kuwa Team Gunner. Endelea kufatilia shaffihdauda.co.tz ili upate habari zaidi kuhusu huyu mchezaji na Arsenal.
2D5909AD00000578-3270063-image-a-49_1444691962804

No comments:

Post a Comment