Saturday, October 3, 2015

Ronaldo atuzwa mpira wa kiatu cha 'madini' kwa kuweka rekodi Real Madrid


MWANASOKA bora wa dunia, Cristiano Ronaldo amefanyiwa pati la kuweka rekodi ya kuwa mfungaji bora wa kihistoria wa Real Madrid katika sherehe zilizofanyika Uwanja wa Santiago Bernabeu na kuhudhuriwa na wachezji wenzake.
Ronaldo aliyevishutumu vyombo vya habari kwa kumsakama, alijumuika na wachezaji wenzake kama Gareth Bale, Karim Benzema na Marcelo waliompogeza Mreno huyo mwenye umri wa miaka 30 katika pati ambayo mama yake, pamoja na mwanawe na wakala wake, Jorge Mendes walihudhuria pia.
Pamoja na hayo taarifa rasmi zinasema Ronaldo amefikia rekodi ya mfungaji bora wa kihistoria wa klabu hiyo, Raul aliyefunga mabao 323 sawa na Ronaldo
 




Ronaldo akiwa na mama yake, Dolores huku mwanawe Cristiano Ronaldo Jr akishuhudia wakati akipokea tuzo yake kiatu na mpira wa Fedha

No comments:

Post a Comment