Wednesday, October 28, 2015

Hans Poppe afunguka kuhusu 'hirizi ya Pape N'Daw


Pape N'daw 
Wenyekiti wa kamati ya usajili ya Simba Zacharia Hans Poppe ameamua kufunguka juu ya mchezaji raia wa Senegal, Pape Abdoulaye N’daw ambaye amekuwa na vituko katika siku za hivi karibuni, miongoni mwa matukio yake ya kukumbukwa ni pamoja na kuingia uwanjani akiwa amevaa viatu vibovu wakati Simba ilipocheza na Yanga.
Lakini kimbwanga kingine ilikuwa ni kutuhumiwa kuwa na hirizi kwenye mechi iliyopita wakati Simba ilipolala kwa goli 1-0 mbele ya Tanzania Prisons kwenye uwanja wa Sokoine, jijini Mbeya.
“Unajua wachezaji wengi wanakuwa na vituko mbalimbali lakini pia waandishi wa habari sasahivi naona wamekuwa wanaropoka-ropoka sana kwasababu huyo N’daw hakuwa na hirizi yoyote ila alikuwa amevaa ‘vest’ flan ndani ambayo ni nyeusi”, amesema Poppe.
Pape Nd'aw
“Alikwenda kukaguliwa na kamisaa na akarudi uwanjani, sasa watu wanaandika kwenye magazeti bila hata kuwa na uhakika hata kusubiri ripoti ya kaimisaa na mwamuzi inasemaje. Hakuwa na hirizi, alikuwa amevaa tu nguo tofauti kidogo na wachezaji wa Prisons walikuwa wanafikiria anahirizi”.
“Unajua kwenye mpira wanasema usivae kitu ambacho kitakuwa hatarishi kwa wenzio, na hakuwa na kitu chochote zaidi ya nguo ya kawaida”.

No comments:

Post a Comment