Wednesday, October 14, 2015

Samatta awania tuzo ya mwanasoka bora Afrika


MSHAMBULIAJI wa kimataifa wa Tanzania, Mbwana Ally Samatta kwa mara ya pili ameingia kwenye kinyang’anyiro cha tuzo ya Mwanasoka Bora wa Mwaka Anayecheza Afrika.
Kwa mujibu wa taarifa ya Shirikisho la Soka Afrika (CAF) imetoa orodha zote mbili za Mwanasoka Bora wa Mwaka Afrika na Mwanasoka Bora wa Mwaka Anayecheza Afrika.
Katika tuzo ya Mwanasoka Bora wa Mwaka Anayecheza Afrika, Samaatta mwenye umri wa miaka 23 anachezea TP Mazembe ya DRC, anachuana na Abdeladim Khadrouf wa Moghreb Tetouan ya nyumbai, Morocco, Abdelmalek Ziaya wa ES SETIF ya nyumbani, Algeria, Ahmed Akaichi wa Esperance ya nyumbani, Tunisa, Andiramahitsinoro Carolus wa Madagascar anayechezea USMA ya Algeria na Baghdad Bounedjah wa Algeria anayechezea Etoile du Sahel ya Tunisia.

Wengine ni Bakri el Madina wa El Merriekh ya nyumbani, Sudan, Bassem Morsi wa Zamalek ya nyumbani, Misri, Boris Moubhio wa AC. Leopards ya nyumbani, Kongo-Brazzaville, Djigui Diarra wa Stade Malien ya nyumbani, Mali na Felipe Ovono wa Guinea anayechezea Orlando Pirates ya Afrika Kusini.
Wamo pia Guelassiognon Sylvain
Gbohouo wa Ivory Coast anayecheza na Samatta T.P Mazembe, Hazem Emam wa Zamalek ya nyumbani, Misri, Hocine Ragued wa Esperance ya nyumnbani, Tunisia, Kermit Erasmus wa Orlando Pirates ya nyumbani Afrika Kusini na Malick Evouna wa Gabon, anayechezea Al Ahly ya Misri.
Wamo pia Mohamed Koffi wa Burkina Faso anayechezea Zamalek ya Misri, Mohamed Meftah wa USMA ya nyumbani, Algeria, Moudather el Tahir wa El Hilal ya nyumbani, Sudan, Oupa Manyisa wa Orlando Pirates ya nyumbani Afrika Kusini, Robert Kidiaba wa T.P Mazembe ya nyumbani, DRC, Roger Assale wa Ivory Coast anayechezea T.P Mazembe, Thamsanqa Gabuza wa Orlando Pirates ya nyumbani Afrika Kusini na 
Zein Edin Farahat wa USMA ya nyumbani, Algeria.
Katika tuzo Ya Mwanasoka Bora wa Mwaka Afrika, Yaya Toure wa Ivory Coast na Manchester City ataitetea dhidi ya Ahmed Musa wa CSKA Moscow ya Urusi na Nigeria, Andre Ayew wa Swansea City ya England na Ghana, Aymen Abdennour wa FC Valence ya Hispania na Tunisia, Baghdad Bonjah wa Etoile du Sahel ya Tunisia na Algeria.
Wengine ni Bassem Morsi wa Zamalek ya Misri, Chrisitian Atsu wa Bournemouth ya England na Ghana, Dieu Merci Mbokani wa Norwich ya England na DRC, El Arbi Hillel Soudani wa Dynamo Zagreb ya Croatia na Algeria, Faouzi Ghoulam wa Napoli ya Italia na Algeria na Ferebory Dore wa Angers ya Ufaransa na Kongo.
Yaya Toure ateteta tuzo yake ya Mwanasoka Bora wa Afrika

 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
Wamo pia Gervais Yao Kouassi wa Rome ya Italia na Ivory Coast, Ibrahima Traore wa Borussia Monchengladbach ya Ujerumani na Guinea, Javier Balboa wa Al-Faisaly ya Saudi Arabia na Equatorial Guinea, Heldon Ramos wa Rio Ave ya Ureno na Cape Verde, Mame Diouf wa Stoke City ya England na Senegal.
Wamo pia Max Alain Gradel wa Bournemouth ya England na Ivory Coast, Mehdi Benatia wa Bayern Munich ya Ujerumani na Morocco, Modather Al Tayeb “Karika” wa El Hilal ya Sudan, Mohamed Salah wa AS Roma ya Italia na Misri, Nicolas Nkoulou wa Marseille ya Ufaransa na Cameroon na Pierre-Emerick Aubameyang wa Borussia Dortmund ya Ujerumani na Gabon.
Wengine ni Robert Kidiaba wa T.P Mazembe, 
Rudy Gestede wa Aston Villa ya England na Benin, Riyad Mahrez wa Leicester City ya England na Algeria, Sadio Mane wa Southampton ya England na Senegal, Serge Aurier wa Paris Saint Germain ya Ufaransa na Ivory Coast na Seydou Keita wa Rome ya Italia na Mali.
Wengine ni Sofiane Feghouli wa Valencia ya Hispania na Algeria, Stephane Mbia wa Trabzonspor ya Uturuki na Cameroon, Thievy Bifouma wa Granada ya Hispania na Kongo, Victor Wanyama wa Southampton ya England na Kenya na Vincent Aboubakar wa Porto ya Ureno na Cameroon.
Wengine ni Vincent Enyeama wa Lille ya Ufaransa na Nigeria, Yacine Brahimi wa Porto ya Ureno na Algeria, Yannick Bolasie wa Crystal Palace ya England na DRC na Yasine Chikhaoui wa Al-Gharafa ya Qatar na Tunisia.

No comments:

Post a Comment