Wednesday, October 28, 2015

Algeria yaweka kikosi hadharani cha kuivaa Stars


Algeria
Algeria tayari imetangaza kikosi cha awali cha wachezaji 32 kitakachoivaa timu ya taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’ kwa ajili ya mchezo wa kuwania kufuzu kucheza fainali za kombe la dunia zitakazofanyika mwaka 2018 nchini Urusi.
Stars na Algeria zitachuana Novemba 14 mwaka huu kwenye uwanja wa taifa jijini Dar es Salaam ukiwa ni mchezo wa kwanza kabla ya kurudiana siku tatu baadae nchini Algeria.
Kuelekea mchezo, Algeria ‘Mbweha wa Jangwani’ imewaita wachezaji wake wengi wanaocheza soka la kulipwa kwenye vilabu vya Ulaya ikiwa ni pamoja na kiungo kinda Bentaleb anayekipika kwenye klabu ya Tottenham, Marhez Riyad na Adlane Guedioura wanaocheza kwenye vilabu vya Leicester na Watford vya England.
Wengine waliojumuishwa kwenye kikosi hicho ni pamoja na Brahimi Yassine (Porto), Sofiane Feghouli (Valencia), Slimani Islam (Sporting Lisbon), Abeid Mehdi (Panathinaicos), Ryad Boudebouz (Montpellier), Saphir Taider (Bologna) na Zeffane Mehdi (Rennes).
Wengine Benrhama Said (Nice), Soudani Hilal Al Arabi (Dinamo Zagreb), Mesbah Djamel Eddine ni (Sampdoria), Rachid Ghezzal (Lyon) and Walid Mesloub (Lorient).
Taifa Stars ilifuzu kucheza raundi ya pili baada ya kuiondosha Malawi kwa wastani wa goli 2-1 kwenye raundi ya awali ya kuwania kufuzu kucheza michuano ya kombe la dunia kufuatia ushindi wa nyumbani wa Stars wa goli 2-0 huku ikipoteza mchezo wake wa ugenini (Malawi) kwa goli 1-0.

No comments:

Post a Comment