Saturday, October 17, 2015

Ni balaa Ligi Kuu Tanzania Bara

MECHI ZA LIGI KUU YA VODACOM TANZANIA BARA WIKIENDI HII
Okotba 17, 2015
Yanga SC Vs Azam FC
Majimaji FC Vs African Sports
Mbeya City Vs Simba SC
Ndanda FC Vs Toto Africans
Stand United Vs Prisons
Coastal Union Vs Mtibwa Sugar
Oktoba 18, 2015
Mgambo Shooting Vs Kagera Sugar
Mwadui FC Vs JKT Ruvu

REKODI YA SIMBA SC NA MBEYA CITY LIGI KUU

April 18, 2015
Mbeya City 2-0 Simba   
Januari 28, 2015
Simba 1-2 Mbeya City     
Februari 15, 2014
Mbeya City 1-1 Simba      
Septemba 21, 2013
Simba 2-2 Mbeya City 
MBEYA City FC leo wanaanza rasmi maisha bila kocha wao, Juma Mwambusi aliyehamia Yanga SC- watakapomenyana na wakongwe, Simba SC katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara Uwanja wa Taifa Dar es Salaam.
Mbeya City inakutana na Simba SC ikiwa na maumivu mara mbili, kwanza kumpoteza kocha wake, Mwambusi aliyekwenda kuwa Msaidizi wa Mholanzi, Hans van der Pluijm Yanga SC na pia, Nahodha wake Juma Nyosso aliyefungiwa miaka miwili.
Lakini habari njema tu ni kwamba, leo inaweza kumtumia kwa mara ya kwanza mchezaji wake mpya, Haruna Moshi Shaaban ‘Boban’ aliyewahi kuchezea Simba SC.
Boban amesajiliwa na Mbeya City msimu huu, lakini akachelewa kujiunga na kikosi kwa sababu ambazo hazijulikani kabla ya wiki hii kutambulishwa amejiunga na timu.
Kocha Muingereza wa Simba SC, Dylan Kerr leo akakosa huduma ya kinara wake wa mabao, Mganda Hamsi Kizza ‘Diego’ ambaye ni majeruhi, lakini Nahodha Mussa Hassan Mgosi yuko tayari kwa mchezo huo.
Msimu huu, Simba SC inaonekana kuwa vizuri kuliko Mbeya City, kwani imepoteza mechi moja tu dhidi ya mahasimu wao, Yanga SC wakati timu ya Mbeya imeshinda mechi moja tu, ikitoa sare moja na kufungwa mara nne.
Kati ya mechi hizo, moja imefungwa nyumbani na Kagera Sugar 1-0 maana yake, si ajabau hata leo wakifungwa na Simba SC nyumbani.   
Lakini ikumbukwe, Simba SC hawajawahi kuifunga Mbeya City tangu ipande Ligi Kuu, msimu wa kwanza wakitoa sare mechi zote na msimu uliopita Wekundu wa Msimbazi wakifungwa mechi zote. 
Je, leo Simba SC iko tayari kufuta uteja kwa Mbeya City? Bila shaka hilo ni jambo la kusubiri na kuona. 

No comments:

Post a Comment