Wednesday, October 28, 2015

Fifa yathibitisha majina saba ya wagombea urais

FIFA
Shirikisho la soka dunia FIFA limetoa orodha ya wagombea wa kinyang’aniro cha Urais wa shrikisho hilo katika uchaguzi utakaofanyika tarehe ya 26 mwezi wa pili 2016.
Katika majina hayo wamo Prince Ali Bin Hussein wa Jordan,Musa Bility wa Liberia,mkurugenzi wa zamani wa masuala ya uhusiano wa kimataifa wa FIFA Jerome Champagne toka nchini Ufaransa,Katibu mkuu wa UEFA Gianni Infantino raia wa Uswisi,Rais wa UEFA Michel Platini , Sheikh Salman Bin Ebrahim Al Khalifa wa Bahrain na Mosima Gabriel maarufu kama ‘Tokyo Sexwale’ wa Afrika Kusini.
Rais wa Shirikisho la soka barani Ulaya ataendelea kuwepo katika kinyang’anyiro hicho mpaka hapo kamati ya maadili ya FIFA itakapotolea majibu ya rufaa ya kiongozi huyo wa soka barani Ulaya.
Lakini kamati ya uchaguzi wa FIFA imesema kuwa haitomweka katika kinyang’anyiro cha Urais Michel Platini mpaka adhabu yake itakapotenguliwa na kamati ya maadili ya FIFA.
Kwa sasa Michel Platini amefungiwa kutojihusisha na soka kwa muda wa siku 90.

No comments:

Post a Comment