Saturday, October 3, 2015

Miaka 19 ya Wenger kuiongoza Arsenal

Wiki hii kwa mara nyingine tena, Arsenal ilionekana kupata taabu kuhimili mikimikiki ya soka la ulaya. Vipigo viwili mfululizo kwenye michuano hiyo vimewaweka kwenye matatizo makubwa. Nafasi yao ya kushika uongozi kwenye kundi lao ilikuwa tayari ngumu lakini sasa haionekani hata kama watafanikiaa kufuzu.   
Arsenal wamekuwa na rekodi mbaya katika michuano ya ulaya kwa muda sasa. Katika msimu mitano iliyopita wametolewa kwenye raundi ya 16.
 
Tangu walipomaliza wakiwa wa washindi wa pili msimu wa 2005/06, wamefika nusu fainali mara moja, robo fainali mara mbili na mara zote zilizobaki waliishia raundi ya 16. Hii ni rekodi ya kikosi cha hadhi ya kati, sio klabu kubwa barani ulaya. Ni vigumu kuiita Arsenal klabu kubwa barani ulaya wakati rekodi yao katika michuano mikubwa ya ulaya imekuwa ya kuchechemea chini ya uongozi wa Wenger.

Hata katika msimu wa 05/06 ilikuwa wazi kwamba haikuwa rahisi kwa wao kutwaa uchampion na kwenye fainali wakiwa -0 uwanjani walifungwa na kikosi bora cha FC Barcelona. Rekodi za Arsenal barani ulaya zinaonesha namna Wenger alivyoshindwa kupambana na vigogo wengine barani humo. Pamoja na kusifiaa nchini England, rekodi zake za ulaya zinaonesha uwezo wake wa kuongoza na kuifundisha Gunners umeshindwa kumudu soka la ulaya.
Labda Wenger sasa ameifikisha Arsenal mahala ambapo inabidi ampe kijiti mwalimu mwingine, kufeli kushindwa kubeba taji lolote kubwa tangu kikosi chake kilipotwaa EPL bila kufungwa msimu wa 2003/04, Arsenal imekwama. Makombe mawili ya FA Cup bado hayakidhi haja bila uwepo wa taji la EPL au lolote la ulaya.
 
Arsenal, katika ardhi yanyumbani bado hawaonekani kama wataupata ubingwa hivi karibuni. Wenger ameunda kikosi chenye wachezaji wanaolipwa fedha nyingi sana –  usajili wa fedha nyingi wa Alexis Sanchez na Mesut Ozili haujaimarisha timu ipasavyo. Timu inakosa wachezaji wanatakaoleta tija kwenye maeneo yenye udhaifu ambao kwa miaka zaidi ya mitano umeendelea kuwa tatizo kwenye timu. – hasa katika nafasi ya kiungo na ulinzi. Lakini udhaifu huu bado haujashughulikiwa inavyopaswa. Je Wenger bado ni mtu sahihi amwa kuipeleka Arsenal hatua nyingine au ndio ameshindwa kabisa kukubaliana na ushindani mpya wa Chelsea na Manchester City.

No comments:

Post a Comment