Wednesday, October 28, 2015

Hans Poppe afunguka kuhusu 'hirizi ya Pape N'Daw


Pape N'daw 
Wenyekiti wa kamati ya usajili ya Simba Zacharia Hans Poppe ameamua kufunguka juu ya mchezaji raia wa Senegal, Pape Abdoulaye N’daw ambaye amekuwa na vituko katika siku za hivi karibuni, miongoni mwa matukio yake ya kukumbukwa ni pamoja na kuingia uwanjani akiwa amevaa viatu vibovu wakati Simba ilipocheza na Yanga.
Lakini kimbwanga kingine ilikuwa ni kutuhumiwa kuwa na hirizi kwenye mechi iliyopita wakati Simba ilipolala kwa goli 1-0 mbele ya Tanzania Prisons kwenye uwanja wa Sokoine, jijini Mbeya.
“Unajua wachezaji wengi wanakuwa na vituko mbalimbali lakini pia waandishi wa habari sasahivi naona wamekuwa wanaropoka-ropoka sana kwasababu huyo N’daw hakuwa na hirizi yoyote ila alikuwa amevaa ‘vest’ flan ndani ambayo ni nyeusi”, amesema Poppe.
Pape Nd'aw
“Alikwenda kukaguliwa na kamisaa na akarudi uwanjani, sasa watu wanaandika kwenye magazeti bila hata kuwa na uhakika hata kusubiri ripoti ya kaimisaa na mwamuzi inasemaje. Hakuwa na hirizi, alikuwa amevaa tu nguo tofauti kidogo na wachezaji wa Prisons walikuwa wanafikiria anahirizi”.
“Unajua kwenye mpira wanasema usivae kitu ambacho kitakuwa hatarishi kwa wenzio, na hakuwa na kitu chochote zaidi ya nguo ya kawaida”.

Rekodi zilizowekwa kwenye Ligi mbalimbali Ulaya mwishoni mwa wiki



MUNICH, Ujerumani
NCHINI Ujerumani, klabu ya Bayern Munich ilipata ushindi wake wa 1000 tangu kuanzishwa kwa ligi hiyo ya Bundesliga baada ya kuifunga FC Koln kwa mabao 4-0.
Katika mchezo huo, golikipa wa Bayern Munich, Manuel Neur aliweka rekodi ya kucheza mchezo wa 138 bila bila kuruhusu wavu wake kutikiswa.
Mchezaji mwingine wa klabu hiyo Arjen Roben aliweka rekodi ya kufunga bao lake la 75 katika ligi ya Bundesliga.
Mshambuliaji wa klabu ya Borussia Dortmund, Pierre Emerick amekuwa mchezaji pekee kutoka klabu ya Dortmund kufunga magoli 13 kwenye mechi 10 ndani ya ligi ya Bundesliga baada ya kufunga magoli matatu (hat-trick) katika ushindi wa Dortmund wa goli 5-1 ilipocheza dhidi ya FC Augsburg.

ITALIA
Klabu ya AS Roma imekwea kileleni mwa Serie A baada ya kupata ushindi wa magoli 2-0 na hiyo inakuwa mara ya kwanza kwa klabu hiyo kukaa kileleni tangu ilipofanya hivyo kwa mara ya mwisho kwenye msimu wa 2013-2014.
Kipa wa AC Milan, Gianluig Donnarumma ameweka rekodi ya kuwa kipa mdogo kucheza mchezo wa Serie A wakati timu yake ilipopata ushindi wa goli 2-1 dhidi ya Sousoro. Bonaroma alidaka kwenye mechi hiyo akiwa na umri wa miaka 16 miezi 8 na siku 6.

UFARANSA
PSG wameendeleza ushindi baada ya ushindi wa goli 4-1 dhidi ya ASSE na kuendelea kukaa kileleni mwa ligi ya Ufaransa.
Mpaka sasa PSG hawajapoteza hata mchezo mmoja kwenye ligi hiyo msimu huu huku timu hiyo ikiwa haijaungwa tangu mwezi Machi mwaka huu tangu walipofungwa na Bodeaux goli 3-2.
Klabu ya Olympic Marseille imepata ushindi wa kwanza kwenye Ligue 1baada ya michezo saba kufuatia ushindi dhidi ya klabu ya Lille wa goli 2-1.

HISPANIA
Baada ya kumshuhudia, Luis Suarez akifunga magoli matatu kwenye ushindi wa goli 3-1 dhidi ya Eibar, kocha wa Barcelona, Luis Enrique Martínez amesema hakuna wa kuziba nafasi ya Suarez hivi sasa.
Ilikuwa ni siku nzuri kwa Suarez kwani alikua akitimiza mwaka mmoja tangu acheze mchezo wake wa kwanza dhidi ya Real Madrid Oktoba 25 2014 katika uwanja wa Santiago Bernabeu.
Hiyo ilikuwa ni hat-trick ya pili kwa Suarez wakati hat-trick ya kwanza ilikuwa ni dhidi ya Cordoba katika ushindi wa Barcelona wa magoli 8-0 msimu uliopita.

ENGLAND
Jurgen Klopp alikuwa akiiongoza Liverpool kwenye mchezo wa kwanza wa ligi ya England katika uwanja wa Unfield dhidi ya Southampton, katika mchezo huo timu hizo zilitoka sare ya kufungana goli 1-1.
Liverpool imefunga magoli tisa tu msimu huu ikiwa timu ya tatu kwa kufunga magoli machache msimu huu ikizizidi klabu za West Brom na Watford pekee ambazo zimefunga magoli nane.
Klabu ya Sunderland imefunga maoli matatu kwa mara ya kwanza tangu tarehe 3 Novemba, 2014. Sunderland iliifunga Newcastle United kwa goli 3-0.
Goli la sekunde ya 49 lililofungwa na Matt Ritchie katika mchezo kati ya Bournemouth dhidi ya Tottenham linakuwa goli la mapema zaidi kwenye msimu wa ligi kuu England. Katika mchezo huo Bournemouth walifungwa goli 5-1 wakiwa kwenye uwanja wao wa nyumbani.
Harry Kane alifunga hat-trick yake ya pili kwenye Ligi Kuu England, alifanya hivyo dhidi ya Leicester City msimu uliopita.

Ratiba Ligi Kuu Tanzania Bara



Oktoba 28, 2015
Toto African Vs Mgambo Shooting
Mwadui FC Vs Yanga SC
Mtibwa Sugar Vs Kagera Sugar
Mbeya City Vs Majimaji FC
Ndanda FC Vs Stand United
Simba SC Vs Coastal Union
Oktoba 29, 2015
JKT Ruvu Vs Azam FC 
Prisons Vs African Sports

MCHEZAJI bora wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara mwezi Septemba, Hamisi Friday Kizza ‘Diego’ yuko tayari kurudi uwanjani leo.
Mganda huyo hajaonekana uwanjani tangu Simba SC ifungwe 2-0 na mahasimu, Yanga SC, Septemba 26, mwaka huu Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, lakini leo anaweza kurudi.
Simba SC inamenyana na Coastal Union ya Tanga katika mfululizo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara leo Uwanja wa Taifa na Ofisa Habari wa Simba SC, Hajji Sunday Manara amesema Kizza anaweza kurudi.
“Kama mchezaji yuko fiti na amefanya mazoezi kikamilifu kuelekea mchezo huu, sasa ni jukumu la kocha mwenyewe kumuanzisha au la. Maana kocha wetu (Muingereza Dylan Kerr) naye ana maamuzi yake,”amesema.
Mbali na Kizza, Manara amesema hata kiungo wao, Jonas Mkude naye yuko vizuri kabisa kuelekea mchezo wa leo na wanamuachia Kerr mwenyewe kama kawaida yake aamue wachezaji wa kutumia.
Kwa ujumla Manara amesema Simba SC haina mchezaji majeruhi wala mgonjwa kuelekea mchezo wa leo na wanasubiri kuona kocha Kerr atawapangia timu ya aina gani leo.
Kwa ujumla, Ligi Kuu inaendelea leo, mbali na Simba na Coastal- Mwadui FC inaikaribisha Yanga SC Uwanja wa Kambarage, Shinyanga, Toto Africans watakuwa wenyeji wa Mgambo Shooting Uwanja wa CCM Kirumba, Mwanza na Mtibwa Sugar watakuwa wenyeji wa ndugu zao Kagera Sugar Uwanja wa Manungu, Turiani, Morogoro. 
Mbeya City watakuwa wenyeji wa Majimaji FC Uwanja wa Sokoine, Ndanda FC wataikaribisha Stand United Uwanja wa Nangwanda, Mtwara wakati kesho JKT Ruvu watamenyana na Azam FC Uwanja wa Karume, Dar es Salaam na Prisons wataikaribisha African Sports Uwanja wa Mkwakwani, Tanga.

Thierry Henry amtaja mchezaji Ligi Kuu England

Scholes 1
Gwiji la soka na mchezaji wa zamani wa Arsenal na timu ya taifa ya Ufaransa, Thierry Henry amewashangaza wengi kwa kumtaja kiungo wa zamani wa England na Manchester United, Paul Scholes kuwa ndiye bora amewahi kukutana naye katika historia ya premier league.
Akijibu swali katika interview moja na Sky Sport, alipotakiwa kumtaja mchezaji bora wa muda wote wa ligi kuu England, tofauti na mashabiki wengi ambao wamekua wakiwapa vipaumbele akina Shearer, Henry mwenyewe, Giggs na Cristiano Ronaldo, lakini nahodha huyo wa zamani wa Arsenal amemtaja Paul Scholes kuwa hana mfano wake.
Scholes
Henry anasema Paul Scholes ndiye mchezaji pekee aliyeweza kuufanya mpira chochote na kwamba kwa mujibu wa Henry, Scholes amekua hapati heshima na sifa anazostahili.
“Paul Scholes ni bora zaidi mimi kuwahi kukutana naye. Timu ya taifa haikutambua ubora wake, lakini Manchester United waliutumia uwezo wake vizuri”.
Scholes 2
Xavi Hernandez wa Barcelona anatajwa kuwa ndiye kiungo bora zaidi kwa miaka kumi, aliwahi kusema kuwa kama yeye ni bora kwa miaka kumi, basi Scholes ni kwa miaka 20.
Scholes 3
Xavi anasema alikua akiongea na Alonso mara nyingi na kwamba Paul Scholes ni miongoni mwa wachezaji bora zaidi wa kizazi chake. Xavi anasema Scholes anaweza kupiga pasi za goli, ndefu na fupi huku akiwa na uwezo mkubwa sana wa ku-control temper ya mchezo.
SPT-GCK-210604- Euro 2004 Portugal England V Croatia Picture Graham Chadwick Scholes goal


Matokeo yote ya mechi za Capital One

Capital One Cup 1
Usiku wa Jumanne nchini England kulipingwa michezo minne ya kombe la Capital One, michezo mitatu kati ya minne iliamuliwa kwa changamoto ya mikwaju ya penati baada ya michezo yote mitatu kumalizika kwa sare ya kufungana goli 1-1.
Sheffield Wednesday wakapata ushindi wa goli 3-0 mbele ya Arsenal na kuing’oa Arsenal kwenye kombe la kwanza msimu huu.
Chelsea dhidi ya Stoke Cty mchezo uliopigwa kwenye uwanja wa Britania Stoke ikafanikiwa kuivua ubingwa Chelsea baada ya kuifunga kwa mikwaju ya penati 5-4 kufuatia sare ya kufungana goli 1-1. Walters aliifungia Stoke City goli la kuongoza dakika ya 52 lakini Loic Remy akaisawazishia Chelsea dakika ya 90.
Eden Hazard akakosa mkwaju wa penati wa mwisho baada ya dakika 120 za mchezo na kuhitimisha safari ya Chelsea kwenye michuano ya Capita One Cup.
Hull City waliwakaribisha Leicester City, Abel Hernandez aliifungia Hull City bao lakini  Riyad Mahrez akaifungia Leicester City bao la kusawazisha na kuufanya mchezo huo kuchezwa kwa dakika 120 na kumalizika kwa matokeo hayo ya kufungana bao 1-1.
Kwenye changamoto ya mikwaju ya penati, Hull City wakafanikiwa kusonga mbele baada ya Riyad Mahrez kukosa penati yake.
Kwenye uwanja wa Goodson Park Everton waliwakaribisha Norwich City mchezo uliomalizika kwa sare ya kufungana goli 1-1. Zikaongezwa dakika 30 lakini bado timu hizo hazikufuyngana, ikabidi itumike mikwaju ya penati kumpata mshindi na Everton wakafanikiwa kusonga mbele.
Capital One Cup results


Fifa yathibitisha majina saba ya wagombea urais

FIFA
Shirikisho la soka dunia FIFA limetoa orodha ya wagombea wa kinyang’aniro cha Urais wa shrikisho hilo katika uchaguzi utakaofanyika tarehe ya 26 mwezi wa pili 2016.
Katika majina hayo wamo Prince Ali Bin Hussein wa Jordan,Musa Bility wa Liberia,mkurugenzi wa zamani wa masuala ya uhusiano wa kimataifa wa FIFA Jerome Champagne toka nchini Ufaransa,Katibu mkuu wa UEFA Gianni Infantino raia wa Uswisi,Rais wa UEFA Michel Platini , Sheikh Salman Bin Ebrahim Al Khalifa wa Bahrain na Mosima Gabriel maarufu kama ‘Tokyo Sexwale’ wa Afrika Kusini.
Rais wa Shirikisho la soka barani Ulaya ataendelea kuwepo katika kinyang’anyiro hicho mpaka hapo kamati ya maadili ya FIFA itakapotolea majibu ya rufaa ya kiongozi huyo wa soka barani Ulaya.
Lakini kamati ya uchaguzi wa FIFA imesema kuwa haitomweka katika kinyang’anyiro cha Urais Michel Platini mpaka adhabu yake itakapotenguliwa na kamati ya maadili ya FIFA.
Kwa sasa Michel Platini amefungiwa kutojihusisha na soka kwa muda wa siku 90.

Algeria yaweka kikosi hadharani cha kuivaa Stars


Algeria
Algeria tayari imetangaza kikosi cha awali cha wachezaji 32 kitakachoivaa timu ya taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’ kwa ajili ya mchezo wa kuwania kufuzu kucheza fainali za kombe la dunia zitakazofanyika mwaka 2018 nchini Urusi.
Stars na Algeria zitachuana Novemba 14 mwaka huu kwenye uwanja wa taifa jijini Dar es Salaam ukiwa ni mchezo wa kwanza kabla ya kurudiana siku tatu baadae nchini Algeria.
Kuelekea mchezo, Algeria ‘Mbweha wa Jangwani’ imewaita wachezaji wake wengi wanaocheza soka la kulipwa kwenye vilabu vya Ulaya ikiwa ni pamoja na kiungo kinda Bentaleb anayekipika kwenye klabu ya Tottenham, Marhez Riyad na Adlane Guedioura wanaocheza kwenye vilabu vya Leicester na Watford vya England.
Wengine waliojumuishwa kwenye kikosi hicho ni pamoja na Brahimi Yassine (Porto), Sofiane Feghouli (Valencia), Slimani Islam (Sporting Lisbon), Abeid Mehdi (Panathinaicos), Ryad Boudebouz (Montpellier), Saphir Taider (Bologna) na Zeffane Mehdi (Rennes).
Wengine Benrhama Said (Nice), Soudani Hilal Al Arabi (Dinamo Zagreb), Mesbah Djamel Eddine ni (Sampdoria), Rachid Ghezzal (Lyon) and Walid Mesloub (Lorient).
Taifa Stars ilifuzu kucheza raundi ya pili baada ya kuiondosha Malawi kwa wastani wa goli 2-1 kwenye raundi ya awali ya kuwania kufuzu kucheza michuano ya kombe la dunia kufuatia ushindi wa nyumbani wa Stars wa goli 2-0 huku ikipoteza mchezo wake wa ugenini (Malawi) kwa goli 1-0.